Tazama kadi zote zilizoangaliwa zaidi kwenye Noor Gallery. ..
Tazama uteuzi wa kadi za kila siku
Qur’an haimzingatii mwanaadam kwa namba tu ya kuhesabika katika huu ulimwengu, bali inamzingatia kuwa ni kiumbe mwenye lengo maalumu la kuumbwa kwake na mwenye ujumbe maalumu
Kila mashindano duniani yana lengo maalumu. Je,inawezekanaje kiakili iwe maisha ya mwanaadam pekee hapa duniani yawe bila maana (lengo)?
“Je! Mlidhani ya kwambatulikuumbeni bure tu
Mwanaadam ni kiumbe wa thamani ambaye haitakiwi kudharauliwa kwa utu wake, au rangi yake au mji wake. Thamani yake ni kubwa kuliko kitu chochote kinachoundwa
Katika kombe la dunia, kuna tofauti ya rangi, lugha na nchi, lakini wote hao wanabaki katika ubinaadam wao. Basi, tambua kuwa Qur’an inatukumbusha kulinda heshima ya kila mtu.
“Na hakika tumewatukuza wanaadam
Uislamu haukutaki kutokuwa na udhaifu, bali unakutaka kujua ni nani wa kumtegemea unapo dhoofika
Nyuma ya nguvu tunazoziona kwenye michezo mbali mbali, kuna mwanadam anaye choka na kuwa na hofu na kudhoofika. Na Qur’an inamzungumzia mwanadam katika hali ukweli na huruma kuhusu maumbile yake.
“Na mwanadam ameumbwa dhaifu
Hata katika nyakati ngumu, fahamu daima kuwa hupatikana uwanda wa faraja wenye nuru. Na huu ndio ujumbe tunaokumbushwa na Qur’an tukufu
Mchezaji wakati mwingine anashindwa kwenye mashindano, kisha anarudi tena kwa nguvu kubwa. Hivyo hivyo, hata mwanadam anaweza kuanza upya katika harakati zake za maisha anapokutana na changamoto yoyote. Tambua kuwa Qur’an haijaufunga mlango wa matumaini, hivyo usikate tamaa!
“Hakika pamoja na uzito upo wepesi