Tazama kadi zote zilizoangaliwa zaidi kwenye Noor Gallery. ..
Tazama uteuzi wa kadi za kila siku
Uongofu unaweza kukufikia kwa ghafla, na ukabadilisha kila kitu baada ya hapo. MAZINGATIO: Qur’an ni nuru ya imani
Muda mfupi tu wa kushikamana na haki, ulibadilisha historia ya wachawi, wakawa ni miongoni mwa waumini wenye kusujudu na kumuabudu Allah. MAZINGATIO: Ni muhimu kuzingatia visa vyenye uongofu
Unapo mchagua Allah kiukweli ina maanisha unakuwa umejipa uhuru wa kutokuwa mtumwa kwa yoyote. MAZINGATIO: Ni wajibu kuwa na tawhidi
Uongofu unaanza wakati moyo unapo fuata haki kwa dhati, na bila kujali kipindi cha ukamiifu wa ufahamu.
Qur’an haikutelekezi katikati ya njia, bali ina ambatana nawe mpaka mwisho na kukupa utulivu wa kweli. MAZINGATIO: Utulivu wa kweli upo ndani ya Qur’an
Hakuna dhiki yoyote inayopatikana katika moyo isipokuwa Qur’an inayo ubainifu wake, au muongozo, au rehema. MAZINGATIO: Qur’an ni muongozo na rehema
Qur’an haihamasishi dhuluma, bali inakutoa kwenye giza la dhuluma hatua kwa hatua na kukupeleka katika nuru ya haki na uongofu. MAZINGATIO: Qur’an ni nuru ya yakini.
Ujumbe wa Qur’an haubadilishi tu anuani, bali unamuokoa mwanaadam kutokana na ujinga. MAZINGATIO: Ujumbe wa Qur’an ni suluhisho la matatizo yote.
Wakati changamoto zinapo kuzonga,hauhitaji kutaabika, bali unahitaji kupata nuru inayo kuangazia na kukuongoza katika kutatua changamoto hizo. MAZINGATIO: Qur’an inaongoa katika njia ya haki
Qur’an siyo majibu yaliyo andaliwa tu, bali ni nuru inayo ambatana nawe hali ya kuwa nawe unaitafuta. MAZINGATIO: Qur’an ni nuru ya uongofu
Allah anapo kupenda, utapata thabati na huto ogopa lawama yoyote, na wala hutoibadilisha haki. MAZINGATIO: Kuthibiti kwa imani kunapatikana kwa kumpenda Allah
Heshima kubwa ya Mwanaadam ni yeye kuwa mwenye kupendeza mbele ya Allah, kabla ya kupendwa na yeye. MAZINGATIO: Allah huwapenda waumini, nao wanampenda