Tazama kadi zote zilizoangaliwa zaidi kwenye Noor Gallery. ..
Tazama uteuzi wa kadi za kila siku
Baada ya kuisha mashindano na makelele, mwanaadam hubaki peke yake pamoja na moyo wake tu(kifo), na wakati huo maswali kuhusu ukweli wa maisha yake aliyo yaishi dunini huanza
Umaarufu,kupiga kelele za makofi, na mashindano mbali mbali, vyote hivyo huwa ni vivutio vya kuteka nyoyo za watu kwa haraka, lakini havidumu daima.
“Na maisha ya dunia si kitu il ani starehe ya udanganyifu
Katika kipindi cha upweke au hofu, Qur’an inazungumza jinsi Allah alivyo karibu na mwanaadam, hivyo asikate tamaa na rehema zake!
Mamilioni ya watu hushuhudia mashindano mbali mbali kutokea maeneo tofauti tofauti ya dunia. Lakini mwanaadam anabakia kuwa na haja ya kupata anayemsikia na kumfahamu kweli katika mihangaiko yake.
“Naye yupo pamoja nanyi popote mlipo
Qur’an inamkumbusha mwanaadam kitu ambacho hukisahu sana anapojishughulisha: kwamba safari ni fupi, na maana halisi ya uhai ni muhimu kuizingatia kuliko kujishughulisha na mihangaiko yenye kumalizika ghafla
Mashindano yoyote yana upeo na ukomo wake. Na uhai pia upo hivyo hivyo, hakuna kisicho kuwa na mwisho.
“Kisha kwa Mola wenu Mlezi mtarejeshwa
Baadhi ya ushindi hauji kwa haraka. Na katika maisha hli ni hivyo hivyo, subira ni sehemu ya safari ya mafanikio.
Watu wengi wanamuheshimu mchezaji anayepambana bila kujisalimisha kirahisi rahisi. Na Qur’an pia inamfundisha mwanaadam namna ya kusubiri katika changamoto mbalimbali na kuendelea na njia ya mafanikio bila kukata tamaa!
“Hakika Allah yu pamoja na wanao subiri