Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Tazama kadi
Kila Aya katika Qur’an imebeba ujumbe maalumu. Na kila mwenye kuitumia akili yake na moyo wake katika kuizingatia Qur’an basi atapata nuru na elimu ya ufahamu wa mambo. MAZINGATIO: Nuru ya Qur’an inaangaza daima
Enyi mlioamini, ombeni msaada kwa uvumilivu (subra) na kuswali. Bila shaka, Allah yupo pamoja na wenye uvumilivu
Unaweza kufikiwa na hali ya dhiki, na ikakukosesha katika dunia hii sehemu ya mali yako na roho za uwapendao. Lakini, mwenye kusubiri na kuridhia qadar ya Allah kwa majaribio hayo, basi hupata bishara njema ya kufanikiwa kutoka kwa Mola wake Mlezi! MAZINGATIO: Subira ni nuru katika maisha
Hakuna katika dunia kitu kikubwa sana kuliko kumkumbuka Allah. Ni nuru ya nyoyo, na kinga ya nafsi, na ngazi ya kuthibiti katika haki. Kila unapomkumbuka na kumtaja Allah kwa dhati ya ukweli kabisa, basi utakuwa karibu yake sana! MAZINGATIO: Kumkumbuka Allah ni jambo kubwa sana.
Je! ni nyoyo ngapi zilizo jiweka mbali na kumkumbuka Allah, mpaka zikawa ngumu na kususuwaa, hali ya kuwa bado wito wa Allah, Mola Mlezi wa viumbe unawaita na kuzitaka zirudi katika unyenyekevu. Je! haujafika wakati kwa nyoyo hizo kunyenyekea? MAZINGATIO: Umuhimu wa kuzizindua nyoyo kutokana na kujisahau, katika kumkumbuka Allah
Katika vipindi vya misiba, haitakiwi kusema sema maneno ya upuuzi! bali inatosha tu kuzingatia kwa Yakini na kurejea maneno mazuri kwa kusema: “Sisi ni wa Allah, na kwake Yeye tutarejea” ndani ya maneno hayo ndiyo ishara ya kujisalimisha kwa Allah na kuridhia qadar yake na kupata utulivu wa nafsi. MAZINGATIO: Umuhimu wa kujisalimisha na kurejea k...