Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Tazama kadi
Allah ndiye aliye muumba mwanaadam. Naye ndiye aliye mfundisha namna ya kujieleza na kuwasiliana. Je, tunazitumia neema za elimu ya ubainifu tulio pewa katika mambo yanayo mridhisha Yeye? MAZINGATIO: Ni wajibu kuikumbuka neema ya ubainifu tuliyo pewa na Allah katika mambo anayo yaridhia
Je! Hawaizingatii hii Qur’ani? Au kwenye nyoyo (zao) zipo kufuli?
Bishara kubwa kwa waumini si kwenye maneno tu, bali pia kwenye ahadi kutoka kwa Allah ya kupata malipo makubwa kwa kila muumini mwenye kufuata njia ya wema. MAZINGATIO: Bishara njema ya kufanikiwa kwa Waumini watendao mema
Moyo uliyo fungwa kwa matamanio hauwezi kufikiwa na nuru ya Qur’an. Na ufunguo wake ni: kuzingatia, kunyenyekea, na kuwa mkweli wa kuitafuta haki. MAZINGATIO: Ufungue moyo wako kwa Qur’an.
Allah hamtelekezi mwenye kusubiri, bali huwa pamoja naye katika dhiki zake na masikitiko yake yanayomtoa machozi, na katika kila sijda anayo ifanya mja mwema huwa kuna matarajio makubwa ya msaada wa Allah. MAZINGATIO: Allah yu pamoja na wanao subiri
Nyoyo ndiyo zinazo fahamu, siyo masikio. Basi, yeyote mwenye kuufungua moyo wake kwa kuifuata haki, atapata katika Qur’an nuru. Na mwenye kuufunga moyo wake, basi hautosikia chochote, hata kama atasomewa Aya zote. MAZINGATIO: Nyoyo ndiyo husikia na kuzingatia.