Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Tazama kadi
Enyi mlioamini, ombeni msaada kwa uvumilivu (subra) na kuswali. Bila shaka, Allah yupo pamoja na wenye uvumilivu
(Allah) Mwingi wa rehmaAmefundisha Qur’aniAmemumba mwanadamuAmemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)
Kujaribiwa si ishara ya kuchukiwa na Allah, bali ni fursa ya kupanda daraja la juu kwa wenye subira. Khofu, njaa, na upungufu wa vitu mbali mbali, vyote hivyo ni masomo muhimu katika kumuamini Allah Mtukufu. MAZINGATIO: Ni wajibu kujifunza katika majaribio na kuwa na subira
Na lau tungelifanya Qur’ani kwa lugha ya kigeni wangelisema: Kwanini Aya zake hazikupambanuliwa? Yawaje lugha ya kigeni na Mtume Mwaarabu? Sema: Hii Qur’ani ni uongofu na ponyo kwa wenye kuamini. Na wasio amini umo uziwi katika masikio yao, nayo kwao imezibwa hawaioni. Hao wanaitwa nao wako pahala pa mbali
Allah hamtelekezi mwenye kusubiri, bali huwa pamoja naye katika dhiki zake na masikitiko yake yanayomtoa machozi, na katika kila sijda anayo ifanya mja mwema huwa kuna matarajio makubwa ya msaada wa Allah. MAZINGATIO: Allah yu pamoja na wanao subiri
Nyoyo ndiyo zinazo fahamu, siyo masikio. Basi, yeyote mwenye kuufungua moyo wake kwa kuifuata haki, atapata katika Qur’an nuru. Na mwenye kuufunga moyo wake, basi hautosikia chochote, hata kama atasomewa Aya zote. MAZINGATIO: Nyoyo ndiyo husikia na kuzingatia.