Je! Hawaizingatii hii Qur’ani? Au kwenye nyoyo (zao) zipo kufuli?
Tazama kadi
Soma uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini kumtaja Allah ndilo jambo kubwa kabisa. Na Allah anayajua mnayo yatenda
Kujaribiwa si ishara ya kuchukiwa na Allah, bali ni fursa ya kupanda daraja la juu kwa wenye subira. Khofu, njaa, na upungufu wa vitu mbali mbali, vyote hivyo ni masomo muhimu katika kumuamini Allah Mtukufu. MAZINGATIO: Ni wajibu kujifunza katika majaribio na kuwa na subira
Kujisahau kunasababisha nyoyo kuwa ngumu. Na kumkumbuka Allah kunazilainisha nyoyo na kuzihuisha upya. Usisubiri kufunikwa na dunia, bali rudi hivi sasa kwa Allah na umuabudu Yeye tu! MAZINGATIO: Ni wajibu kurejea kwa Allah kwa kumkumbuka.
Wakati unapo fikwa na majanga, usitafute ufumbuzi wa nje kwanza. Bali rudi kwenye Subira na Sala, ndani yake kuna msaada mkubwa wa kutoka mbinguni kwa Allah. MAZINGATIO: Umuhimu wa kushikamana na Subira na Sala
Na lau tungelifanya Qur’ani kwa lugha ya kigeni wangelisema: Kwanini Aya zake hazikupambanuliwa? Yawaje lugha ya kigeni na Mtume Mwaarabu? Sema: Hii Qur’ani ni uongofu na ponyo kwa wenye kuamini. Na wasio amini umo uziwi katika masikio yao, nayo kwao imezibwa hawaioni. Hao wanaitwa nao wako pahala pa mbali
Enyi mlioamini, ombeni msaada kwa uvumilivu (subra) na kuswali. Bila shaka, Allah yupo pamoja na wenye uvumilivu