Je! Hawaizingatii hii Qur’ani? Au kwenye nyoyo (zao) zipo kufuli?
Tazama kadi
Moyo uliyo fungwa kwa matamanio hauwezi kufikiwa na nuru ya Qur’an. Na ufunguo wake ni: kuzingatia, kunyenyekea, na kuwa mkweli wa kuitafuta haki. MAZINGATIO: Ufungue moyo wako kwa Qur’an.
Qur’an siyo Kitabu kinacho somwa tu. Bali ni Kitabu cha kuzingatiwa! Yeyote asiye zingatia maana yake, ana kuwa kama mtu ambaye moyoni mwake kuna kufuli lisilo funguka! MAZINGATIO: Ni wajibu kuizingatia Qur’an Tukufu
Je, haujafika wakati kwa walioamini kwamba zinyenyekee nyoyo zao kwa kumuabudu Allah na yale yaliyoteremka ya haki, na wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla ya hapo, na ukarefuka juu yao muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? Na wengi miongoni mwao ni mafasiki
Hakika hii Qur’ani inaongoa kwenye yale yaliyo nyooka kabisa, na inawabashiria Waumini ambao wanatenda mema ya kwamba watapata malipo makubwa
Soma uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini kumtaja Allah ndilo jambo kubwa kabisa. Na Allah anayajua mnayo yatenda
Qur’an husomwa ili kuzifundisha nyoyo maadili mema. Na Sala husimamishwa ili kuzisafisha nafsi ziwe na tabia njema. Basi, mwenye kudumisha mafungamano yake na Mola wake Mlezi, atapata ulinzi wake wa kutokuwa na maadili mabaya. MAZINGATIO: Athari ya Sala katika maisha ya mtu na jamii