Je! Hawaizingatii hii Qur’ani? Au kwenye nyoyo (zao) zipo kufuli?
Tazama kadi
Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Kila Aya katika Qur’an imebeba ujumbe maalumu. Na kila mwenye kuitumia akili yake na moyo wake katika kuizingatia Qur’an basi atapata nuru na elimu ya ufahamu wa mambo. MAZINGATIO: Nuru ya Qur’an inaangaza daima
Qur’an imekuwa ni neema ya kwanza baada ya rehema za Allah. Na inatufunza kuwa neema kubwa aliyo fundishwa mwanaadam baada ya kuumbwa kwake ni kupewa ujuzi wa maneno ya Allah (Qur’an). MAZINGATIO: Qur’an ni rehema.
Na kwa yakini kabisa, tutakutieni katika mtihani mdogo wa hofu na njaa na upungufu wa mali na uhai na matunda. Na wape bishara wenye uvumilivu
Katika vipindi vya misiba, haitakiwi kusema sema maneno ya upuuzi! bali inatosha tu kuzingatia kwa Yakini na kurejea maneno mazuri kwa kusema: “Sisi ni wa Allah, na kwake Yeye tutarejea” ndani ya maneno hayo ndiyo ishara ya kujisalimisha kwa Allah na kuridhia qadar yake na kupata utulivu wa nafsi. MAZINGATIO: Umuhimu wa kujisalimisha na kurejea k...
Kujaribiwa si ishara ya kuchukiwa na Allah, bali ni fursa ya kupanda daraja la juu kwa wenye subira. Khofu, njaa, na upungufu wa vitu mbali mbali, vyote hivyo ni masomo muhimu katika kumuamini Allah Mtukufu. MAZINGATIO: Ni wajibu kujifunza katika majaribio na kuwa na subira