Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Tazama kadi
Kila Aya katika Qur’an imebeba ujumbe maalumu. Na kila mwenye kuitumia akili yake na moyo wake katika kuizingatia Qur’an basi atapata nuru na elimu ya ufahamu wa mambo. MAZINGATIO: Nuru ya Qur’an inaangaza daima
Je! Hawaizingatii hii Qur’ani? Au kwenye nyoyo (zao) zipo kufuli?
Qur’an husomwa ili kuzifundisha nyoyo maadili mema. Na Sala husimamishwa ili kuzisafisha nafsi ziwe na tabia njema. Basi, mwenye kudumisha mafungamano yake na Mola wake Mlezi, atapata ulinzi wake wa kutokuwa na maadili mabaya. MAZINGATIO: Athari ya Sala katika maisha ya mtu na jamii
Hakika hii Qur’ani inaongoa kwenye yale yaliyo nyooka kabisa, na inawabashiria Waumini ambao wanatenda mema ya kwamba watapata malipo makubwa
Na lau tungelifanya Qur’ani kwa lugha ya kigeni wangelisema: Kwanini Aya zake hazikupambanuliwa? Yawaje lugha ya kigeni na Mtume Mwaarabu? Sema: Hii Qur’ani ni uongofu na ponyo kwa wenye kuamini. Na wasio amini umo uziwi katika masikio yao, nayo kwao imezibwa hawaioni. Hao wanaitwa nao wako pahala pa mbali
Bishara kubwa kwa waumini si kwenye maneno tu, bali pia kwenye ahadi kutoka kwa Allah ya kupata malipo makubwa kwa kila muumini mwenye kufuata njia ya wema. MAZINGATIO: Bishara njema ya kufanikiwa kwa Waumini watendao mema