Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Tazama kadi
Allah hamtelekezi mwenye kusubiri, bali huwa pamoja naye katika dhiki zake na masikitiko yake yanayomtoa machozi, na katika kila sijda anayo ifanya mja mwema huwa kuna matarajio makubwa ya msaada wa Allah. MAZINGATIO: Allah yu pamoja na wanao subiri
Moyo uliyo fungwa kwa matamanio hauwezi kufikiwa na nuru ya Qur’an. Na ufunguo wake ni: kuzingatia, kunyenyekea, na kuwa mkweli wa kuitafuta haki. MAZINGATIO: Ufungue moyo wako kwa Qur’an.
Je, haujafika wakati kwa walioamini kwamba zinyenyekee nyoyo zao kwa kumuabudu Allah na yale yaliyoteremka ya haki, na wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla ya hapo, na ukarefuka juu yao muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? Na wengi miongoni mwao ni mafasiki
Na kwa yakini kabisa, tutakutieni katika mtihani mdogo wa hofu na njaa na upungufu wa mali na uhai na matunda. Na wape bishara wenye uvumilivu
Na lau tungelifanya Qur’ani kwa lugha ya kigeni wangelisema: Kwanini Aya zake hazikupambanuliwa? Yawaje lugha ya kigeni na Mtume Mwaarabu? Sema: Hii Qur’ani ni uongofu na ponyo kwa wenye kuamini. Na wasio amini umo uziwi katika masikio yao, nayo kwao imezibwa hawaioni. Hao wanaitwa nao wako pahala pa mbali
Qur’an siyo Kitabu kinacho somwa tu. Bali ni Kitabu cha kuzingatiwa! Yeyote asiye zingatia maana yake, ana kuwa kama mtu ambaye moyoni mwake kuna kufuli lisilo funguka! MAZINGATIO: Ni wajibu kuizingatia Qur’an Tukufu