Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Tazama kadi
Nyoyo ndiyo zinazo fahamu, siyo masikio. Basi, yeyote mwenye kuufungua moyo wake kwa kuifuata haki, atapata katika Qur’an nuru. Na mwenye kuufunga moyo wake, basi hautosikia chochote, hata kama atasomewa Aya zote. MAZINGATIO: Nyoyo ndiyo husikia na kuzingatia.
Je! ni nyoyo ngapi zilizo jiweka mbali na kumkumbuka Allah, mpaka zikawa ngumu na kususuwaa, hali ya kuwa bado wito wa Allah, Mola Mlezi wa viumbe unawaita na kuzitaka zirudi katika unyenyekevu. Je! haujafika wakati kwa nyoyo hizo kunyenyekea? MAZINGATIO: Umuhimu wa kuzizindua nyoyo kutokana na kujisahau, katika kumkumbuka Allah
Qur’an ina kuongoa kwenye njia iliyo nyooka. Si kwa maamrisho tu na makatazo, bali ni muongozo wa maisha yako yote kwa kukupa mafanikio na utukufu. MAZINGATIO: Qur’an ni muongozo wa maisha.
Kujaribiwa si ishara ya kuchukiwa na Allah, bali ni fursa ya kupanda daraja la juu kwa wenye subira. Khofu, njaa, na upungufu wa vitu mbali mbali, vyote hivyo ni masomo muhimu katika kumuamini Allah Mtukufu. MAZINGATIO: Ni wajibu kujifunza katika majaribio na kuwa na subira
Na lau tungelifanya Qur’ani kwa lugha ya kigeni wangelisema: Kwanini Aya zake hazikupambanuliwa? Yawaje lugha ya kigeni na Mtume Mwaarabu? Sema: Hii Qur’ani ni uongofu na ponyo kwa wenye kuamini. Na wasio amini umo uziwi katika masikio yao, nayo kwao imezibwa hawaioni. Hao wanaitwa nao wako pahala pa mbali
Qur’an siyo Kitabu kinacho somwa tu. Bali ni Kitabu cha kuzingatiwa! Yeyote asiye zingatia maana yake, ana kuwa kama mtu ambaye moyoni mwake kuna kufuli lisilo funguka! MAZINGATIO: Ni wajibu kuizingatia Qur’an Tukufu