Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Tazama kadi
Allah ndiye aliye muumba mwanaadam. Naye ndiye aliye mfundisha namna ya kujieleza na kuwasiliana. Je, tunazitumia neema za elimu ya ubainifu tulio pewa katika mambo yanayo mridhisha Yeye? MAZINGATIO: Ni wajibu kuikumbuka neema ya ubainifu tuliyo pewa na Allah katika mambo anayo yaridhia
Allah hamtelekezi mwenye kusubiri, bali huwa pamoja naye katika dhiki zake na masikitiko yake yanayomtoa machozi, na katika kila sijda anayo ifanya mja mwema huwa kuna matarajio makubwa ya msaada wa Allah. MAZINGATIO: Allah yu pamoja na wanao subiri
Je! ni nyoyo ngapi zilizo jiweka mbali na kumkumbuka Allah, mpaka zikawa ngumu na kususuwaa, hali ya kuwa bado wito wa Allah, Mola Mlezi wa viumbe unawaita na kuzitaka zirudi katika unyenyekevu. Je! haujafika wakati kwa nyoyo hizo kunyenyekea? MAZINGATIO: Umuhimu wa kuzizindua nyoyo kutokana na kujisahau, katika kumkumbuka Allah
Soma uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini kumtaja Allah ndilo jambo kubwa kabisa. Na Allah anayajua mnayo yatenda
Hakuna katika dunia kitu kikubwa sana kuliko kumkumbuka Allah. Ni nuru ya nyoyo, na kinga ya nafsi, na ngazi ya kuthibiti katika haki. Kila unapomkumbuka na kumtaja Allah kwa dhati ya ukweli kabisa, basi utakuwa karibu yake sana! MAZINGATIO: Kumkumbuka Allah ni jambo kubwa sana.
Enyi mlioamini, ombeni msaada kwa uvumilivu (subra) na kuswali. Bila shaka, Allah yupo pamoja na wenye uvumilivu