Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Tazama kadi
Moyo uliyo fungwa kwa matamanio hauwezi kufikiwa na nuru ya Qur’an. Na ufunguo wake ni: kuzingatia, kunyenyekea, na kuwa mkweli wa kuitafuta haki. MAZINGATIO: Ufungue moyo wako kwa Qur’an.
Nyoyo ndiyo zinazo fahamu, siyo masikio. Basi, yeyote mwenye kuufungua moyo wake kwa kuifuata haki, atapata katika Qur’an nuru. Na mwenye kuufunga moyo wake, basi hautosikia chochote, hata kama atasomewa Aya zote. MAZINGATIO: Nyoyo ndiyo husikia na kuzingatia.
Hakuna katika dunia kitu kikubwa sana kuliko kumkumbuka Allah. Ni nuru ya nyoyo, na kinga ya nafsi, na ngazi ya kuthibiti katika haki. Kila unapomkumbuka na kumtaja Allah kwa dhati ya ukweli kabisa, basi utakuwa karibu yake sana! MAZINGATIO: Kumkumbuka Allah ni jambo kubwa sana.
Kila mtihani, huzuni na msiba, kwa hali yoyote iwavyo, itakuwa ni miepesi unapo kumbuka kuwa wewe ni mwenye kurejea kwa aliye kuumba. MAZINGATIO: Umuhimu wa kuwa na mazingatio katika misiba na kushikamana na Subira.
Allah ndiye aliye muumba mwanaadam. Naye ndiye aliye mfundisha namna ya kujieleza na kuwasiliana. Je, tunazitumia neema za elimu ya ubainifu tulio pewa katika mambo yanayo mridhisha Yeye? MAZINGATIO: Ni wajibu kuikumbuka neema ya ubainifu tuliyo pewa na Allah katika mambo anayo yaridhia
Soma uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini kumtaja Allah ndilo jambo kubwa kabisa. Na Allah anayajua mnayo yatenda