Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Tazama kadi
Moyo uliyo fungwa kwa matamanio hauwezi kufikiwa na nuru ya Qur’an. Na ufunguo wake ni: kuzingatia, kunyenyekea, na kuwa mkweli wa kuitafuta haki. MAZINGATIO: Ufungue moyo wako kwa Qur’an.
Qur’an imekuwa ni neema ya kwanza baada ya rehema za Allah. Na inatufunza kuwa neema kubwa aliyo fundishwa mwanaadam baada ya kuumbwa kwake ni kupewa ujuzi wa maneno ya Allah (Qur’an). MAZINGATIO: Qur’an ni rehema.
Wakati unapo fikwa na majanga, usitafute ufumbuzi wa nje kwanza. Bali rudi kwenye Subira na Sala, ndani yake kuna msaada mkubwa wa kutoka mbinguni kwa Allah. MAZINGATIO: Umuhimu wa kushikamana na Subira na Sala
Enyi mlioamini, ombeni msaada kwa uvumilivu (subra) na kuswali. Bila shaka, Allah yupo pamoja na wenye uvumilivu
Kila mtihani, huzuni na msiba, kwa hali yoyote iwavyo, itakuwa ni miepesi unapo kumbuka kuwa wewe ni mwenye kurejea kwa aliye kuumba. MAZINGATIO: Umuhimu wa kuwa na mazingatio katika misiba na kushikamana na Subira.
Nyoyo ndiyo zinazo fahamu, siyo masikio. Basi, yeyote mwenye kuufungua moyo wake kwa kuifuata haki, atapata katika Qur’an nuru. Na mwenye kuufunga moyo wake, basi hautosikia chochote, hata kama atasomewa Aya zote. MAZINGATIO: Nyoyo ndiyo husikia na kuzingatia.