Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Tazama kadi
Enyi mlioamini, ombeni msaada kwa uvumilivu (subra) na kuswali. Bila shaka, Allah yupo pamoja na wenye uvumilivu
Hakika hii Qur’ani inaongoa kwenye yale yaliyo nyooka kabisa, na inawabashiria Waumini ambao wanatenda mema ya kwamba watapata malipo makubwa
Na kwa yakini kabisa, tutakutieni katika mtihani mdogo wa hofu na njaa na upungufu wa mali na uhai na matunda. Na wape bishara wenye uvumilivu
(Allah) Mwingi wa rehmaAmefundisha Qur’aniAmemumba mwanadamuAmemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)
Soma uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini kumtaja Allah ndilo jambo kubwa kabisa. Na Allah anayajua mnayo yatenda
Wakati unapo fikwa na majanga, usitafute ufumbuzi wa nje kwanza. Bali rudi kwenye Subira na Sala, ndani yake kuna msaada mkubwa wa kutoka mbinguni kwa Allah. MAZINGATIO: Umuhimu wa kushikamana na Subira na Sala