(Allah) Mwingi wa rehma
Amefundisha Qur’ani
Amemumba mwanadamu
Amemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)
Tazama kadi
Qur’an imekuwa ni neema ya kwanza baada ya rehema za Allah. Na inatufunza kuwa neema kubwa aliyo fundishwa mwanaadam baada ya kuumbwa kwake ni kupewa ujuzi wa maneno ya Allah (Qur’an). MAZINGATIO: Qur’an ni rehema.
Unaweza kufikiwa na hali ya dhiki, na ikakukosesha katika dunia hii sehemu ya mali yako na roho za uwapendao. Lakini, mwenye kusubiri na kuridhia qadar ya Allah kwa majaribio hayo, basi hupata bishara njema ya kufanikiwa kutoka kwa Mola wake Mlezi! MAZINGATIO: Subira ni nuru katika maisha
Nyoyo ndiyo zinazo fahamu, siyo masikio. Basi, yeyote mwenye kuufungua moyo wake kwa kuifuata haki, atapata katika Qur’an nuru. Na mwenye kuufunga moyo wake, basi hautosikia chochote, hata kama atasomewa Aya zote. MAZINGATIO: Nyoyo ndiyo husikia na kuzingatia.
Bishara kubwa kwa waumini si kwenye maneno tu, bali pia kwenye ahadi kutoka kwa Allah ya kupata malipo makubwa kwa kila muumini mwenye kufuata njia ya wema. MAZINGATIO: Bishara njema ya kufanikiwa kwa Waumini watendao mema
Kila mtihani, huzuni na msiba, kwa hali yoyote iwavyo, itakuwa ni miepesi unapo kumbuka kuwa wewe ni mwenye kurejea kwa aliye kuumba. MAZINGATIO: Umuhimu wa kuwa na mazingatio katika misiba na kushikamana na Subira.
Hakika hii Qur’ani inaongoa kwenye yale yaliyo nyooka kabisa, na inawabashiria Waumini ambao wanatenda mema ya kwamba watapata malipo makubwa