(Allah) Mwingi wa rehma
Amefundisha Qur’ani
Amemumba mwanadamu
Amemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)
Tazama kadi
Qur’an siyo Kitabu kinacho somwa tu. Bali ni Kitabu cha kuzingatiwa! Yeyote asiye zingatia maana yake, ana kuwa kama mtu ambaye moyoni mwake kuna kufuli lisilo funguka! MAZINGATIO: Ni wajibu kuizingatia Qur’an Tukufu
Qur’an haikuteremshwa kwa ajili ya mapambo wala kupata baraka tu, bali imeteremshwa ili tuifahamu na kuizingatia, na kufuata muongozo wake katika kila jambo. MAZINGATIO: Ni wajibu kuizingatia Qur’an Tukufu
Allah hamtelekezi mwenye kusubiri, bali huwa pamoja naye katika dhiki zake na masikitiko yake yanayomtoa machozi, na katika kila sijda anayo ifanya mja mwema huwa kuna matarajio makubwa ya msaada wa Allah. MAZINGATIO: Allah yu pamoja na wanao subiri
Kila mtihani, huzuni na msiba, kwa hali yoyote iwavyo, itakuwa ni miepesi unapo kumbuka kuwa wewe ni mwenye kurejea kwa aliye kuumba. MAZINGATIO: Umuhimu wa kuwa na mazingatio katika misiba na kushikamana na Subira.
Hakuna katika dunia kitu kikubwa sana kuliko kumkumbuka Allah. Ni nuru ya nyoyo, na kinga ya nafsi, na ngazi ya kuthibiti katika haki. Kila unapomkumbuka na kumtaja Allah kwa dhati ya ukweli kabisa, basi utakuwa karibu yake sana! MAZINGATIO: Kumkumbuka Allah ni jambo kubwa sana.
Je! Hawaizingatii hii Qur’ani? Au kwenye nyoyo (zao) zipo kufuli?