(Allah) Mwingi wa rehma
Amefundisha Qur’ani
Amemumba mwanadamu
Amemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)
Tazama kadi
Na kwa yakini kabisa, tutakutieni katika mtihani mdogo wa hofu na njaa na upungufu wa mali na uhai na matunda. Na wape bishara wenye uvumilivu
Qur’an imekuwa ni neema ya kwanza baada ya rehema za Allah. Na inatufunza kuwa neema kubwa aliyo fundishwa mwanaadam baada ya kuumbwa kwake ni kupewa ujuzi wa maneno ya Allah (Qur’an). MAZINGATIO: Qur’an ni rehema.
Unaweza kufikiwa na hali ya dhiki, na ikakukosesha katika dunia hii sehemu ya mali yako na roho za uwapendao. Lakini, mwenye kusubiri na kuridhia qadar ya Allah kwa majaribio hayo, basi hupata bishara njema ya kufanikiwa kutoka kwa Mola wake Mlezi! MAZINGATIO: Subira ni nuru katika maisha
Kila mtihani, huzuni na msiba, kwa hali yoyote iwavyo, itakuwa ni miepesi unapo kumbuka kuwa wewe ni mwenye kurejea kwa aliye kuumba. MAZINGATIO: Umuhimu wa kuwa na mazingatio katika misiba na kushikamana na Subira.
Qur’an ina kuongoa kwenye njia iliyo nyooka. Si kwa maamrisho tu na makatazo, bali ni muongozo wa maisha yako yote kwa kukupa mafanikio na utukufu. MAZINGATIO: Qur’an ni muongozo wa maisha.
Wakati unapo fikwa na majanga, usitafute ufumbuzi wa nje kwanza. Bali rudi kwenye Subira na Sala, ndani yake kuna msaada mkubwa wa kutoka mbinguni kwa Allah. MAZINGATIO: Umuhimu wa kushikamana na Subira na Sala