(Allah) Mwingi wa rehma
Amefundisha Qur’ani
Amemumba mwanadamu
Amemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)
Tazama kadi
Je! ni nyoyo ngapi zilizo jiweka mbali na kumkumbuka Allah, mpaka zikawa ngumu na kususuwaa, hali ya kuwa bado wito wa Allah, Mola Mlezi wa viumbe unawaita na kuzitaka zirudi katika unyenyekevu. Je! haujafika wakati kwa nyoyo hizo kunyenyekea? MAZINGATIO: Umuhimu wa kuzizindua nyoyo kutokana na kujisahau, katika kumkumbuka Allah
Nyoyo ndiyo zinazo fahamu, siyo masikio. Basi, yeyote mwenye kuufungua moyo wake kwa kuifuata haki, atapata katika Qur’an nuru. Na mwenye kuufunga moyo wake, basi hautosikia chochote, hata kama atasomewa Aya zote. MAZINGATIO: Nyoyo ndiyo husikia na kuzingatia.
Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Qur’an ina kuongoa kwenye njia iliyo nyooka. Si kwa maamrisho tu na makatazo, bali ni muongozo wa maisha yako yote kwa kukupa mafanikio na utukufu. MAZINGATIO: Qur’an ni muongozo wa maisha.
Qur’an siyo Kitabu kinacho somwa tu. Bali ni Kitabu cha kuzingatiwa! Yeyote asiye zingatia maana yake, ana kuwa kama mtu ambaye moyoni mwake kuna kufuli lisilo funguka! MAZINGATIO: Ni wajibu kuizingatia Qur’an Tukufu
Allah ndiye aliye muumba mwanaadam. Naye ndiye aliye mfundisha namna ya kujieleza na kuwasiliana. Je, tunazitumia neema za elimu ya ubainifu tulio pewa katika mambo yanayo mridhisha Yeye? MAZINGATIO: Ni wajibu kuikumbuka neema ya ubainifu tuliyo pewa na Allah katika mambo anayo yaridhia