(Allah) Mwingi wa rehma
Amefundisha Qur’ani
Amemumba mwanadamu
Amemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)
Tazama kadi
Je! Hawaizingatii hii Qur’ani? Au kwenye nyoyo (zao) zipo kufuli?
Nyoyo ndiyo zinazo fahamu, siyo masikio. Basi, yeyote mwenye kuufungua moyo wake kwa kuifuata haki, atapata katika Qur’an nuru. Na mwenye kuufunga moyo wake, basi hautosikia chochote, hata kama atasomewa Aya zote. MAZINGATIO: Nyoyo ndiyo husikia na kuzingatia.
Bishara kubwa kwa waumini si kwenye maneno tu, bali pia kwenye ahadi kutoka kwa Allah ya kupata malipo makubwa kwa kila muumini mwenye kufuata njia ya wema. MAZINGATIO: Bishara njema ya kufanikiwa kwa Waumini watendao mema
Allah hamtelekezi mwenye kusubiri, bali huwa pamoja naye katika dhiki zake na masikitiko yake yanayomtoa machozi, na katika kila sijda anayo ifanya mja mwema huwa kuna matarajio makubwa ya msaada wa Allah. MAZINGATIO: Allah yu pamoja na wanao subiri
Katika vipindi vya misiba, haitakiwi kusema sema maneno ya upuuzi! bali inatosha tu kuzingatia kwa Yakini na kurejea maneno mazuri kwa kusema: “Sisi ni wa Allah, na kwake Yeye tutarejea” ndani ya maneno hayo ndiyo ishara ya kujisalimisha kwa Allah na kuridhia qadar yake na kupata utulivu wa nafsi. MAZINGATIO: Umuhimu wa kujisalimisha na kurejea k...
Kujaribiwa si ishara ya kuchukiwa na Allah, bali ni fursa ya kupanda daraja la juu kwa wenye subira. Khofu, njaa, na upungufu wa vitu mbali mbali, vyote hivyo ni masomo muhimu katika kumuamini Allah Mtukufu. MAZINGATIO: Ni wajibu kujifunza katika majaribio na kuwa na subira