(Allah) Mwingi wa rehma
Amefundisha Qur’ani
Amemumba mwanadamu
Amemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)
Tazama kadi
Nyoyo ndiyo zinazo fahamu, siyo masikio. Basi, yeyote mwenye kuufungua moyo wake kwa kuifuata haki, atapata katika Qur’an nuru. Na mwenye kuufunga moyo wake, basi hautosikia chochote, hata kama atasomewa Aya zote. MAZINGATIO: Nyoyo ndiyo husikia na kuzingatia.
Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Kujisahau kunasababisha nyoyo kuwa ngumu. Na kumkumbuka Allah kunazilainisha nyoyo na kuzihuisha upya. Usisubiri kufunikwa na dunia, bali rudi hivi sasa kwa Allah na umuabudu Yeye tu! MAZINGATIO: Ni wajibu kurejea kwa Allah kwa kumkumbuka.
Qur’an husomwa ili kuzifundisha nyoyo maadili mema. Na Sala husimamishwa ili kuzisafisha nafsi ziwe na tabia njema. Basi, mwenye kudumisha mafungamano yake na Mola wake Mlezi, atapata ulinzi wake wa kutokuwa na maadili mabaya. MAZINGATIO: Athari ya Sala katika maisha ya mtu na jamii
Soma uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini kumtaja Allah ndilo jambo kubwa kabisa. Na Allah anayajua mnayo yatenda
Je, haujafika wakati kwa walioamini kwamba zinyenyekee nyoyo zao kwa kumuabudu Allah na yale yaliyoteremka ya haki, na wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla ya hapo, na ukarefuka juu yao muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? Na wengi miongoni mwao ni mafasiki