(Allah) Mwingi wa rehma
Amefundisha Qur’ani
Amemumba mwanadamu
Amemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)
Tazama kadi
Enyi mlioamini, ombeni msaada kwa uvumilivu (subra) na kuswali. Bila shaka, Allah yupo pamoja na wenye uvumilivu
Allah ndiye aliye muumba mwanaadam. Naye ndiye aliye mfundisha namna ya kujieleza na kuwasiliana. Je, tunazitumia neema za elimu ya ubainifu tulio pewa katika mambo yanayo mridhisha Yeye? MAZINGATIO: Ni wajibu kuikumbuka neema ya ubainifu tuliyo pewa na Allah katika mambo anayo yaridhia
Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika, sisi ni wa Allah, na kwake yeye tu tutarejea
Na kwa yakini kabisa, tutakutieni katika mtihani mdogo wa hofu na njaa na upungufu wa mali na uhai na matunda. Na wape bishara wenye uvumilivu
Bishara kubwa kwa waumini si kwenye maneno tu, bali pia kwenye ahadi kutoka kwa Allah ya kupata malipo makubwa kwa kila muumini mwenye kufuata njia ya wema. MAZINGATIO: Bishara njema ya kufanikiwa kwa Waumini watendao mema
Soma uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini kumtaja Allah ndilo jambo kubwa kabisa. Na Allah anayajua mnayo yatenda