(Yusuf) Alisema: Mtalima miaka saba mfululizo[1]. Mtakachovuna kiacheni katika mashuke yake, isipokuwa kidogo mtakachokula
Kisha baada ya miaka saba itakuja miaka (mingine) ya shida[1] (ambapo watu) watakula kile walichokihifadhi isipokuwa kidogo mlichokihifadhi (kwa ajili ya mbegu)
Kisha itakuja baada ya hapo (miaka saba ya neema) mwaka (ambao) katika mwaka huo watu wataokolewa (kwa kuletewa mvua ya neema) na katika mwaka huo watakamua (yale mazao yakamuliwayo)
Kadi zenye uhusiano
Tazama kadi
