“Naye yupo pamoja nanyi popote mlipo
Tazama kadi
Qur’an inamkumbusha mwanaadam kitu ambacho hukisahu sana anapojishughulisha: kwamba safari ni fupi, na maana halisi ya uhai ni muhimu kuizingatia kuliko kujishughulisha na mihangaiko yenye kumalizika ghafla
Qur’an haimzingatii mwanaadam kwa namba tu ya kuhesabika katika huu ulimwengu, bali inamzingatia kuwa ni kiumbe mwenye lengo maalumu la kuumbwa kwake na mwenye ujumbe maalumu
“Hakika pamoja na uzito upo wepesi
Katika kipindi cha upweke au hofu, Qur’an inazungumza jinsi Allah alivyo karibu na mwanaadam, hivyo asikate tamaa na rehema zake!
Mashindano yoyote yana upeo na ukomo wake. Na uhai pia upo hivyo hivyo, hakuna kisicho kuwa na mwisho.
Hata katika nyakati ngumu, fahamu daima kuwa hupatikana uwanda wa faraja wenye nuru. Na huu ndio ujumbe tunaokumbushwa na Qur’an tukufu