Je! Hawaizingatii hii Qur’ani? Au kwenye nyoyo (zao) zipo kufuli?
Tazama kadi
Qur’an husomwa ili kuzifundisha nyoyo maadili mema. Na Sala husimamishwa ili kuzisafisha nafsi ziwe na tabia njema. Basi, mwenye kudumisha mafungamano yake na Mola wake Mlezi, atapata ulinzi wake wa kutokuwa na maadili mabaya. MAZINGATIO: Athari ya Sala katika maisha ya mtu na jamii
Nyoyo ndiyo zinazo fahamu, siyo masikio. Basi, yeyote mwenye kuufungua moyo wake kwa kuifuata haki, atapata katika Qur’an nuru. Na mwenye kuufunga moyo wake, basi hautosikia chochote, hata kama atasomewa Aya zote. MAZINGATIO: Nyoyo ndiyo husikia na kuzingatia.
Kila mtihani, huzuni na msiba, kwa hali yoyote iwavyo, itakuwa ni miepesi unapo kumbuka kuwa wewe ni mwenye kurejea kwa aliye kuumba. MAZINGATIO: Umuhimu wa kuwa na mazingatio katika misiba na kushikamana na Subira.
Hakika hii Qur’ani inaongoa kwenye yale yaliyo nyooka kabisa, na inawabashiria Waumini ambao wanatenda mema ya kwamba watapata malipo makubwa
Bishara kubwa kwa waumini si kwenye maneno tu, bali pia kwenye ahadi kutoka kwa Allah ya kupata malipo makubwa kwa kila muumini mwenye kufuata njia ya wema. MAZINGATIO: Bishara njema ya kufanikiwa kwa Waumini watendao mema
Na kwa yakini kabisa, tutakutieni katika mtihani mdogo wa hofu na njaa na upungufu wa mali na uhai na matunda. Na wape bishara wenye uvumilivu