Je! Hawaizingatii hii Qur’ani? Au kwenye nyoyo (zao) zipo kufuli?
Tazama kadi
Allah hamtelekezi mwenye kusubiri, bali huwa pamoja naye katika dhiki zake na masikitiko yake yanayomtoa machozi, na katika kila sijda anayo ifanya mja mwema huwa kuna matarajio makubwa ya msaada wa Allah. MAZINGATIO: Allah yu pamoja na wanao subiri
Enyi mlioamini, ombeni msaada kwa uvumilivu (subra) na kuswali. Bila shaka, Allah yupo pamoja na wenye uvumilivu
Nyoyo ndiyo zinazo fahamu, siyo masikio. Basi, yeyote mwenye kuufungua moyo wake kwa kuifuata haki, atapata katika Qur’an nuru. Na mwenye kuufunga moyo wake, basi hautosikia chochote, hata kama atasomewa Aya zote. MAZINGATIO: Nyoyo ndiyo husikia na kuzingatia.
Na lau tungelifanya Qur’ani kwa lugha ya kigeni wangelisema: Kwanini Aya zake hazikupambanuliwa? Yawaje lugha ya kigeni na Mtume Mwaarabu? Sema: Hii Qur’ani ni uongofu na ponyo kwa wenye kuamini. Na wasio amini umo uziwi katika masikio yao, nayo kwao imezibwa hawaioni. Hao wanaitwa nao wako pahala pa mbali
Qur’an siyo Kitabu kinacho somwa tu. Bali ni Kitabu cha kuzingatiwa! Yeyote asiye zingatia maana yake, ana kuwa kama mtu ambaye moyoni mwake kuna kufuli lisilo funguka! MAZINGATIO: Ni wajibu kuizingatia Qur’an Tukufu
Soma uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini kumtaja Allah ndilo jambo kubwa kabisa. Na Allah anayajua mnayo yatenda