Uislamu haukutaki kutokuwa na udhaifu, bali unakutaka kujua ni nani wa kumtegemea unapo dhoofika
Tazama kadi
Ulimwengu unawafauatilia wachezaji katika kombe la dunia. Lakini Qur’an inakutaka ujiangalie wewe mwenyewe kwanza.
“Kisha kwa Mola wenu Mlezi mtarejeshwa
Qur’an inamkumbusha mwanaadam kitu ambacho hukisahu sana anapojishughulisha: kwamba safari ni fupi, na maana halisi ya uhai ni muhimu kuizingatia kuliko kujishughulisha na mihangaiko yenye kumalizika ghafla
Mamilioni ya watu hushuhudia mashindano mbali mbali kutokea maeneo tofauti tofauti ya dunia. Lakini mwanaadam anabakia kuwa na haja ya kupata anayemsikia na kumfahamu kweli katika mihangaiko yake.
Baadhi ya ushindi hauji kwa haraka. Na katika maisha hli ni hivyo hivyo, subira ni sehemu ya safari ya mafanikio.
Watu hutafuta furaha katika ushindi. Lakini baadhi ya nyoyo hubakia katika hali ya wasiwasi hata baada ya kushinda, kwa sababu utulivu siyo kombe lenye kubebwa, bali ni amani inayo patikana moyoni.