Sema: Atakufisheni Malaika wa mauti aliye wakilishwa juu yenu; kisha mtarejeshwa kwa Mola wenu Mlezi
Tazama kadi
Enyi miloamini, kuweni wasimamizi (wa haki) kwa ajili ya Allah, mtoao ushahidi kwa uadilifu. Na kuwachukia (watu) kusikupelekeeni kutofanya uadilifu. Fanyeni uadilifu (kwa watu wote). Hilo ndilo lililo karibu zaidi (kufikisha) kwenye uchamungu. Na mcheni Allah. Hakika, Allah anayajua mnayoyatenda
Kwa hakika Allah anaamuru uadilifu, na ihsani, na kuwapa (sadaka) ndugu wa karibu na anakataza uchafu, na uovu, na uasi. Anawanasihini ili mpate kukumbuka
Na simamisheni mzani kwa uadilifu na msipunguze mizani
Siku utakayowaona Waumini wa kiume na Waumini wa kike, nuru zao zinakimbilia mbele yao na kuliani kwao; (wataambiwa): Bishara njema kwenu leo! Ya pepo zipitazo chini yake mito, ni wenye kukaa humo milele. Huko ndiko kufuzu kukubwaSiku wanafiki wa kiume na wanafiki wa kike watakapowaambia wale walioamini: Tungojeeni, tupate mwangaza kutokana na nuru...
Hakika, Allah Hadhulumu uzito wa punje. Na kama (uzito huo wa punje) ni jambo zuri analizidisha na anatoa ujira mkubwa kabisa kutoka kwake
Hakika amefanikiwa aliye itakasa, Na hakika amepata hasara aliye iviza (ichafua)