Sema: Atakufisheni Malaika wa mauti aliye wakilishwa juu yenu; kisha mtarejeshwa kwa Mola wenu Mlezi
Tazama kadi
Enyi miloamini, kuweni wasimamizi (wa haki) kwa ajili ya Allah, mtoao ushahidi kwa uadilifu. Na kuwachukia (watu) kusikupelekeeni kutofanya uadilifu. Fanyeni uadilifu (kwa watu wote). Hilo ndilo lililo karibu zaidi (kufikisha) kwenye uchamungu. Na mcheni Allah. Hakika, Allah anayajua mnayoyatenda
Na simamisheni mzani kwa uadilifu na msipunguze mizani
Allah, hakuna anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Yeye tu. Yeye ndiye Mwenye uhai wa milele, Mwenye kusimamia kila kitu. Hapatwi na kusinzia wala kulala. Ni vyake yeye tu vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Ni nani awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao, wala hawajui kitu katika elimu yake is...
Hakika, sisi tumemuongoza (tumempa mwongozo unaofikishwa na Mitume); ama awe mwenye kushukuru au mwenye kukufuru
Kwa hakika Allah anaamuru uadilifu, na ihsani, na kuwapa (sadaka) ndugu wa karibu na anakataza uchafu, na uovu, na uasi. Anawanasihini ili mpate kukumbuka
Hakika amefanikiwa aliye itakasa, Na hakika amepata hasara aliye iviza (ichafua)