Na wale (wenye akili ndio) ambao huyaunga aliyoamrisha Allah yaungwe, na wanaihofu hesabu mbaya
Tazama kadi
Watakapokujia wanafiki wanasema: Tunashuhudia kwamba wewe bila ya shaka yoyote ni Mtume wa Allah. Na Allah Anajua kuwa hakika wewe ni Mtume Wake, na Allah anashuhudia kuwa kwa hakika kabisa wanafiki ni waongo
Wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa Motoni, kwa sababu ya mioyo yao kuficha ukafiri na kudhihirisha imani kwa uongo. Basi, Waislamu wawe na tahadhari kubwa ya kujionesha na kufanya unafiki katika maneno na matendo. Na ni wajibu kuwa na nia ya kweli na kushikamana na imani kwani ndiyo msingi mkuu wa maisha yetu. Tunachojifunza: Tahad...
Allah Mtukufu ametuumba mataifa na makabila mbali mbali ili tujuane sisi kwa sisi. Kutofautiana kimaumbile na kimaeneo ni neema, na si sababu ya kutengana. Bali iwe ni msingi wa kuboresha mahusiano yetu kwa kuheshimiana na kutambuana. Tunachojifunza: Kuishi pamoja kwa amani, na kuthaminiana kibinaadamu ni katika Uislamu.
Na wanapokutana na walioamini wanasema: Tumeamini. Na wanapokuwa faragha na mashetani wao wanasema: Sisi tuko pamoja nanyi, tunachokifanya sisi tunacheza shere tu Allah anawacheza shere wao, na anawapa muda zaidi katika kupotoka kwao huku wakiwa wanatangatanga
Kumfanyia wema jirani ni miongoni mwa tabia njema zilizo sisitizwa na dini yetu tukufu ya Uislamu.Haki za jirani, haziishii kwa jirani aliye ndugu tu, bali zimekusanya hata jirani wa mbali. Hivyo basi, ni wajibu wetu kuzifanya rehema za Allah na uadilifu wake ndiyo msingi wa kuamiliana kwetu katika maisha yetu ya kila siku.Tunachojifunza...
Enyi watu, mcheni Mola wenu Mlezi Ambaye amekuumbeni kutokana na nafsi moja tu na ameumba kutoka kwenye nafsi hiyo mke wake (Hawaa), na akaeneza kutokana na wawili hao wanaume wengi na wanawake (wengi), na mcheni Allah Ambaye mnaombana kupitia yeye, na (ogopeni kukata) udugu. Hakika, Allah amekuwa Mwenye kukufuatilieni kwa karibu sana