Na wale (wenye akili ndio) ambao huyaunga aliyoamrisha Allah yaungwe, na wanaihofu hesabu mbaya
Tazama kadi
Enyi watu, mcheni Mola wenu Mlezi Ambaye amekuumbeni kutokana na nafsi moja tu na ameumba kutoka kwenye nafsi hiyo mke wake (Hawaa), na akaeneza kutokana na wawili hao wanaume wengi na wanawake (wengi), na mcheni Allah Ambaye mnaombana kupitia yeye, na (ogopeni kukata) udugu. Hakika, Allah amekuwa Mwenye kukufuatilieni kwa karibu sana
Na wajizuilie na machafu wale wasiopata cha kuolea, mpaka Allah awatajirishe kwa fadhila yake. Na wanao taka kuandikiwa uhuru katika wale ambao mikono yenu ya kulia imewamiliki, basi waandikieni kama mkiona wema kwao. Na wapeni katika mali ya Allah aliyo kupeni. Wala msiwashurutishe vijakazi wenu kufanya zina kwa ajili ya kutafuta pato la maisha ya...
Watu ambao wanaunganisha yaliyo amrishwa na Allah kuunganishwa, hao ndiyo watapata mafanikio na rehema za Allah. Basi, ni wajibu wetu kudumisha mahusiano mema ya kibinaadamu na kiimani kati yetu, kwani huo ni ufunguo wa kheri na baraka. Tunachojifunza: Kuunga undugu, kuwa na huruma ni katika imani.
Na (kumbukeni) Tulipochukua ahadi kwa Wana wa Israeli kwamba, hamtamuabudu yeyote Ila Allah tu, na mtawatendea wema wazazi, na ndugu na yatima na maskini, na mseme na watu kwa maneno mazuri. Na simamisheni Swala na toeni Zaka, kisha mkakengeuka isipokuwa wachache tu kati yenu, na ilhali nyinyi mnapuuza
Watakapokujia wanafiki wanasema: Tunashuhudia kwamba wewe bila ya shaka yoyote ni Mtume wa Allah. Na Allah Anajua kuwa hakika wewe ni Mtume Wake, na Allah anashuhudia kuwa kwa hakika kabisa wanafiki ni waongo