Na wale (wenye akili ndio) ambao huyaunga aliyoamrisha Allah yaungwe, na wanaihofu hesabu mbaya
Tazama kadi
Watu ambao wanaunganisha yaliyo amrishwa na Allah kuunganishwa, hao ndiyo watapata mafanikio na rehema za Allah. Basi, ni wajibu wetu kudumisha mahusiano mema ya kibinaadamu na kiimani kati yetu, kwani huo ni ufunguo wa kheri na baraka. Tunachojifunza: Kuunga undugu, kuwa na huruma ni katika imani.
Tafakuri ya Nabii Ibrahim- Amani iwe juu yake- katika mbingu na ardhi ilikuwa ndiyo njia yake ya kupata yakini.Mwanaadam kila anapo tazama ukubwa wa viumbe wa Allah humzidishia yakini juu ya uwezo wa Allah na utukufu wake.Hivyo basi, ni wajibu wetu kuziboresha imani zetu kwa kutafakari viumbe wa Allah. Tunachojifunza:Imani ni msingi wa kupata...
Na mwabuduni Allah na msikishirikishe naye kitu chochote. Na wazazi wawili wafanyieni mazuri, na ndugu wa karibu (wa nasaba), na Yatima na maskini na jirani wa karibu (mwenye udugu wa nasaba) na jirani wa mbali (kwa makazi au udugu) na rafiki aliyeko ubavuni (rafiki mwenye usuhuba wa karibu na pia mke) na msafiri (aliyeharibikiwa) na wale walio chi...
Allah Mtukufu ndiye Mjuzi wa viumbe wake, Mjuzi wa kila kitu alicho kiumba, naye ni Mpole, Mwenye khabari za hali zote za kila kiumbe. Basi tujue kuwa hakuna ponyo wala raha isipo kuwa kutoka kwake tu, na ni wajibu wetu kuwa na yakini na hekima zake na rehema zake katika kila jambo. Tunachojifunza: Ujuzi wa Allah juu ya viumbe wake ni mk...
Je, Huwaoni wanao fanya unaafiki na wanawaambia ndugu zao walio kufuru katika Watu wa Kitabu: Mkitolewa na sisi lazima tutatoka pamoja nanyi, wala hatutamt’ii yeyote kabisa dhidi yenu. Na mkipigwa vita lazima tutakusaidieni. Na Mwenyezi Mungu anashuhudia kuwa hakika hao bila ya shaka ni waongo
Kumfanyia wema jirani ni miongoni mwa tabia njema zilizo sisitizwa na dini yetu tukufu ya Uislamu.Haki za jirani, haziishii kwa jirani aliye ndugu tu, bali zimekusanya hata jirani wa mbali. Hivyo basi, ni wajibu wetu kuzifanya rehema za Allah na uadilifu wake ndiyo msingi wa kuamiliana kwetu katika maisha yetu ya kila siku.Tunachojifunza...