Na wale (wenye akili ndio) ambao huyaunga aliyoamrisha Allah yaungwe, na wanaihofu hesabu mbaya
Tazama kadi
Ukweli ni njia ya wokovu Tunatakiwa kushikamana na wakweli, kwani ndiyo salama ya nyoyo zetu na ukweli wa maneno: “ Mcheni Allah, na kuweni pamoja na wakweli” ili muishi maisha yaliyo jaa baraka na uongofu. Tunachojifunza: Umuhimu wa Ukweli, toba na imani
Utakapo waona watu ambao wanafanya upuuzi na shere kwenye Aya za Allah, basi waepuke haraka sana, mpaka waache upuuzi huo na upotevu.Ni wajibu kwako kuilinda imani yako, na wala usishirikiane na ambaye atakupoteza, bali fuata njia ya Uislamu, iliyo nyooka.Tunachojifunza:Kujitenga na upotofu ni katika imani na tawhidi.
Enyi watu tumewaumbeni wanaume na wanawake na tumewafanyeni mataifa na makabila ili mutambuane hakika mbora zaidi wenu kwa Allah ni mcha Mungu zaidi kwenu hakika Allah ni mjuzi mno mwenye habari nyingi
Watakapokujia wanafiki wanasema: Tunashuhudia kwamba wewe bila ya shaka yoyote ni Mtume wa Allah. Na Allah Anajua kuwa hakika wewe ni Mtume Wake, na Allah anashuhudia kuwa kwa hakika kabisa wanafiki ni waongo
Na wajizuilie na machafu wale wasiopata cha kuolea, mpaka Allah awatajirishe kwa fadhila yake. Na wanao taka kuandikiwa uhuru katika wale ambao mikono yenu ya kulia imewamiliki, basi waandikieni kama mkiona wema kwao. Na wapeni katika mali ya Allah aliyo kupeni. Wala msiwashurutishe vijakazi wenu kufanya zina kwa ajili ya kutafuta pato la maisha ya...
Kumfanyia wema jirani ni miongoni mwa tabia njema zilizo sisitizwa na dini yetu tukufu ya Uislamu.Haki za jirani, haziishii kwa jirani aliye ndugu tu, bali zimekusanya hata jirani wa mbali. Hivyo basi, ni wajibu wetu kuzifanya rehema za Allah na uadilifu wake ndiyo msingi wa kuamiliana kwetu katika maisha yetu ya kila siku.Tunachojifunza...