Na wale (wenye akili ndio) ambao huyaunga aliyoamrisha Allah yaungwe, na wanaihofu hesabu mbaya
Tazama kadi
Na mwabuduni Allah na msikishirikishe naye kitu chochote. Na wazazi wawili wafanyieni mazuri, na ndugu wa karibu (wa nasaba), na Yatima na maskini na jirani wa karibu (mwenye udugu wa nasaba) na jirani wa mbali (kwa makazi au udugu) na rafiki aliyeko ubavuni (rafiki mwenye usuhuba wa karibu na pia mke) na msafiri (aliyeharibikiwa) na wale walio chi...
Allah Mtukufu ndiye Mjuzi wa viumbe wake, Mjuzi wa kila kitu alicho kiumba, naye ni Mpole, Mwenye khabari za hali zote za kila kiumbe. Basi tujue kuwa hakuna ponyo wala raha isipo kuwa kutoka kwake tu, na ni wajibu wetu kuwa na yakini na hekima zake na rehema zake katika kila jambo. Tunachojifunza: Ujuzi wa Allah juu ya viumbe wake ni mk...
Enyi watu, mcheni Mola wenu Mlezi Ambaye amekuumbeni kutokana na nafsi moja tu na ameumba kutoka kwenye nafsi hiyo mke wake (Hawaa), na akaeneza kutokana na wawili hao wanaume wengi na wanawake (wengi), na mcheni Allah Ambaye mnaombana kupitia yeye, na (ogopeni kukata) udugu. Hakika, Allah amekuwa Mwenye kukufuatilieni kwa karibu sana
Kufurahi kwetu kwa neema alizo tuneemesha Allah juu yetu ni miongoni mwa fadhila zake na rehema zake, na hivyo ni bora kuliko chochote tunacho kikusanya katika dunia. Ni wajibu wetu kuwa wenye shukurani, na kukumbuka siku zote kuwa radhi za Allah ni neema kubwa. Tunachojifunza: Fadhila za Allah, kuridhia na kuwa na shukurani juu ya neema...
Watu ambao wanaunganisha yaliyo amrishwa na Allah kuunganishwa, hao ndiyo watapata mafanikio na rehema za Allah. Basi, ni wajibu wetu kudumisha mahusiano mema ya kibinaadamu na kiimani kati yetu, kwani huo ni ufunguo wa kheri na baraka. Tunachojifunza: Kuunga undugu, kuwa na huruma ni katika imani.
Sema: Kwa hakika Mola wangu Mlezi humkunjulia riziki na humdhikisha amtakaye katika waja wake. Na chochote mtakacho kitoa Yeye atakilipa. Naye ni Mbora wa wanao ruzuku