Je! Umemwona aliye yafanya matamanio yake kuwa ndio mungu wake? Basi je, wewe utakuwa ni wakili wake?
Tazama kadi
Matamanio huvutia nyoyo kupenda mali, watoto na vipambo vya dunia(wanawake nk) lakini vyote hivyo ni starehe ya muda tu. Ama marejeo mema yapo kwa Allah kwa kila mwenye kutakasa niya na kufanya juhudi. Tunajifunza kuwa: Kutakasa niya, ndiyo mafanikio ya kweli.
Mema na maovu hayalingani. Pinga uovu kwa lilio jema zaidi. Hapo yule ambaye baina yako na baina yake pana uadui atakuwa kama rafiki jamaa wa kukuonea uchungu Lakini hawapewi wema huu ila wanao subiri, wala hawapewi ila wenye bahati kubwa
Katika safari na jihadi, Allah ameruhusu kufupisha sala, kwa lengo la waumini kujilinda na maudhi ya makafiri. Na hii ni rehema ya Uislamu inayo dhihiri katika kuwepesisha ibada katika kipindi kigumu. Tunajifunza kuwa: Kuwepesishwa sala wakati wa dhiki ni huruma ya Uislamu.
Unapokutana na upuuzi na maneno mabaya, basi kumbuka muongozo kuwa Muumini wa kweli huwa anajitenga na hayo na kuchagua salama. Bali inatakiwa kuwa mzuri wa majibu kwa kusema: “Matendo yetu ni yetu, na yenu ni yenu, na sisi Waislamu hatutaki kujibizana na wajinga”. Tunajifunza kuwa: Katika tabia njema ni kujiepusha na batili.
Katika harakati zako za amani na safari, kumbuka kuwa Uislamu ni dini ya huruma na wepesi. Umeruhusu kufupisha sala ikiwa unahofia maudhi ya maadui. Na adui yenu yupo wazi wazi kwa vitimbi vyake, lakini rehema za Allah juu yenu ni pana sana. Tunajifunza kuwa: Kufupisha sala katika vipindi vya dhiki ni katika wepesi wa dini ya Uislam.
Pepo si ya mwenye kuzuia hasira zake tu, bali ni ya mwenye kutoa katika wasaa na dhiki, na akawasamehe watu. Njia za kupata radhi za Allah zipo katika matendo ya wema.Tunajifunza kuwa: Huruma ni katika matendo ya wema.