Je! Umemwona aliye yafanya matamanio yake kuwa ndio mungu wake? Basi je, wewe utakuwa ni wakili wake?
Tazama kadi
Wakati mawimbi yanapo zidi, na hali ya hewa ikawa mbaya baharini, huwa tunauona udhaifu wetu mbele ya uwezo wa Allah, na huwa tunamuelekea Yeye kwa kumuomba kwa ikhlaswi. Lakini balaa kubwa ni pale tunapo okolewa na kuwa salama, kuacha kuonesha shukurani zetu kwa Allah, jambo hili ni baya sana na lisilo faa kufanywa na Waumini wa kweli. Tunajifunz...
Jueni kwamba maisha ya dunia ni mchezo na pumbao na mapambo, na kufakharishana baina yenu na kushindana kwa wingi wa mali na watoto; ni kama mfano wa mvua inayowafurahisha wakulima mimea yake, kisha yananyweya, kisha utayaona yamepiga manjano, kisha yanakuwa mabua. Na Akhera kuna adhabu kali, na msamaha kutoka kwa Allah na radhi zake. Na uhai wa du...
Na ukimbilieni msamaha wa Mola wenu Mlezi na Pepo (ambayo) upana wake ni mbingu na ardhi, iliyoandaliwa kwa ajili ya wacha Mungu (Wacha Mungu) Ambao wanatoa (katika vile walivyopewa na Allah) katika hali ya wasaa na katika hali ya dhiki, na wenye kuzuia hasira (zao) na kusamehe watu (wanaowakosea). Na Allah anawapenda wafanyao mazuri
Na wanapo sikia upuuzi hujitenga nao na husema: Sisi tuna vitendo vyetu, na nyinyi mna vitendo vyenu. Salamun Alaikum, Amani juu yenu! Sisi hatutaki kujibizana na wajinga
Na mnaposafiri ardhini, basi hakuna ubaya wowote kwenu kupunguza Swala ikiwa mtahofia kupata mitihani ya makafiri (kwa kukudhuruni). Hakika makafiri wamekuwa maadui wa dhahiri kwenu
Matamanio huvutia nyoyo kupenda mali, watoto na vipambo vya dunia(wanawake nk) lakini vyote hivyo ni starehe ya muda tu. Ama marejeo mema yapo kwa Allah kwa kila mwenye kutakasa niya na kufanya juhudi. Tunajifunza kuwa: Kutakasa niya, ndiyo mafanikio ya kweli.