Je! Umemwona aliye yafanya matamanio yake kuwa ndio mungu wake? Basi je, wewe utakuwa ni wakili wake?
Tazama kadi
Mema na maovu hayalingani. Kuwa miongoni mwa wale ambao wanalipiza ubaya kwa wema. Huwenda adui yako akabadilika na kuwa rafiki yako kipenzi. Na haya hawayafikii ila walio na subira na wenye bahati kubwa. Tunajifunza kuwa: Wema na subira ni katika tabia njema za Uislamu
Na mnaposafiri ardhini, basi hakuna ubaya wowote kwenu kupunguza Swala ikiwa mtahofia kupata mitihani ya makafiri (kwa kukudhuruni). Hakika makafiri wamekuwa maadui wa dhahiri kwenu
Dunia si chochote ila ni mchezo, na upuuzi na mapambo wanayo jifakharisha nayo watu, na kukithirisha mali na watoto. Mfano wake ni kama mazao yanayo mea na kukauka na hatimaye mtu akajisahau na kujikuta hana kitu huko akhera. Malipo ya huko, ima ni adhabu au msamaha na radhi kutoka kwa Allah. Tunajifunza kuwa: Dunia haidumu, na akhera ndio inayo...
Mapambo ya dunia hii yamezungukwa na mapenzi ya mali, watoto na kuwa na nguvu. Lakini vyote hivyo ni starehe yenye kuisha. Kuhangaikia vilivyo kwa Allah ndiyo lengo kuu, na marejeo bora ya akhera na mafanikio makubwa. Tunajifunza kuwa: Akhera ni bora kuliko dunia isiyo dumu.
Kuukimbilia msamaha wa Allah na Pepo yake aliyo waahidi Waumini, ni neema kubwa ya Allah ambayo humpa amtakaye. Basi, ewe Muumini! Weka lengo lako kuu kuwa ni kufaulu kwa kufanya juhudi zitakazo kuwezesha kupata radhi za Allah na kupata msamaha wake. Tunajifunza kuwa:
Jueni kwamba maisha ya dunia ni mchezo na pumbao na mapambo, na kufakharishana baina yenu na kushindana kwa wingi wa mali na watoto; ni kama mfano wa mvua inayowafurahisha wakulima mimea yake, kisha yananyweya, kisha utayaona yamepiga manjano, kisha yanakuwa mabua. Na Akhera kuna adhabu kali, na msamaha kutoka kwa Allah na radhi zake. Na uhai wa du...