Je! Umemwona aliye yafanya matamanio yake kuwa ndio mungu wake? Basi je, wewe utakuwa ni wakili wake?
Tazama kadi
Jueni kwamba maisha ya dunia ni mchezo na pumbao na mapambo, na kufakharishana baina yenu na kushindana kwa wingi wa mali na watoto; ni kama mfano wa mvua inayowafurahisha wakulima mimea yake, kisha yananyweya, kisha utayaona yamepiga manjano, kisha yanakuwa mabua. Na Akhera kuna adhabu kali, na msamaha kutoka kwa Allah na radhi zake. Na uhai wa du...
Ole wake kila mwenye kufanya matamanio yake ni mungu, na hiyo ndio njia ya upotofu. Tunawajibika sisi kukumbushana na kupeana nasaha, kwani kila mtu ataulizwa kuhusu utashi wake mbele ya Allah. Tunajifunza kuwa: Ni wajibu kulingania haki, na kutahadhari juu ya kufuata matamanio.
Na mnaposafiri ardhini, basi hakuna ubaya wowote kwenu kupunguza Swala ikiwa mtahofia kupata mitihani ya makafiri (kwa kukudhuruni). Hakika makafiri wamekuwa maadui wa dhahiri kwenu
Dunia si chochote ila ni mchezo, na upuuzi na mapambo wanayo jifakharisha nayo watu, na kukithirisha mali na watoto. Mfano wake ni kama mazao yanayo mea na kukauka na hatimaye mtu akajisahau na kujikuta hana kitu huko akhera. Malipo ya huko, ima ni adhabu au msamaha na radhi kutoka kwa Allah. Tunajifunza kuwa: Dunia haidumu, na akhera ndio inayo...
Maisha ya dunia yana onekana wazi kwa mambo ya kupumbaza na upuuzi. Lakini mwisho wake ni kama mwisho wa mazao ambayo huishia kuwa mabua! Kumbuka! Akhera ndio inayo dumu, ima kupata msamaha na radhi za Allah au kupata adhabu kali. Tunajifunza kuwa: Dunia ni starehe zenye kudanganya, na akhera ndio bora.
Matamanio huvutia nyoyo kupenda mali, watoto na vipambo vya dunia(wanawake nk) lakini vyote hivyo ni starehe ya muda tu. Ama marejeo mema yapo kwa Allah kwa kila mwenye kutakasa niya na kufanya juhudi. Tunajifunza kuwa: Kutakasa niya, ndiyo mafanikio ya kweli.