Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi
Tazama kadi
Na namna hivi tumekufunulia Qur’ani kwa amri yetu. Ulikuwa hujui Kitabu ni nini, wala Imani. Lakini tumekifanya kuwa ni Nuru ambayo kwayo tunamwongoa tumtakaye katika waja wetu. Na hakika wewe unaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka
Enyi watu, hakika yamekujieni mawaidha kutoka kwa Mola wenu Mlezi na ponyo (dawa) ya (maradhi) yaliyomo vifuani (mwenu) na muongozo na rehema kwa Waumini
Qur’an haikutelekezi katikati ya njia, bali ina ambatana nawe mpaka mwisho na kukupa utulivu wa kweli. MAZINGATIO: Utulivu wa kweli upo ndani ya Qur’an
Uongofu unaweza kukufikia kwa ghafla, na ukabadilisha kila kitu baada ya hapo. MAZINGATIO: Qur’an ni nuru ya imani
Qur’an haikutoi katika giza moja tu, bali inakutoa katika viza vingi na kukufikisha katika nuru moja tu ya uongofu iliyo wazi. MAZINGATIO: Qur’an inaongoa kutoka katika giza na kupeleka katika nuru
Katika ulimwengu uliofunikwa na giza, Qur’an inakuja kama nuru isiyo kutelekeza, bali inkujulisha njia yenye usalama na amani. MAZINGATIO: Qur’an ndiyo njia ya amani