Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi
Tazama kadi
Qur’an haikutelekezi katikati ya njia, bali ina ambatana nawe mpaka mwisho na kukupa utulivu wa kweli. MAZINGATIO: Utulivu wa kweli upo ndani ya Qur’an
Wakati kifua chako kinapopata dhiki na ukawa hujui ni ipi sababu ya machungu ya dhiki hiyo,yaliyomo ndani yake, basi Qur’an inakuja kukupa suluhisho lake na si kukukaripia. Bali inakuponya maradhi yote uliyo nayo yasiyo onekana kwa macho wala fikra za kawaida. MAZINGATIO: Qur’an ni ponyo la nyoyo
Qur’an haihamasishi dhuluma, bali inakutoa kwenye giza la dhuluma hatua kwa hatua na kukupeleka katika nuru ya haki na uongofu. MAZINGATIO: Qur’an ni nuru ya yakini.
Muda mfupi tu wa kushikamana na haki, ulibadilisha historia ya wachawi, wakawa ni miongoni mwa waumini wenye kusujudu na kumuabudu Allah. MAZINGATIO: Ni muhimu kuzingatia visa vyenye uongofu
Alif Lam Raa . Hiki ni Kitabu tulichokiteremsha kwako ili kwacho uwatowe watu kwenye giza uwapeleke kwenye muangaza, kwa idhini ya Mola wao Mlezi, uwafikishe kwenye Njia ya Mwenye nguvu, Msifiwa
Unapo mchagua Allah kiukweli ina maanisha unakuwa umejipa uhuru wa kutokuwa mtumwa kwa yoyote. MAZINGATIO: Ni wajibu kuwa na tawhidi