Enyi mlio amini! Rukuuni na msujudu, na muabuduni Mola wenu Mlezi, na tendeni mema, ili mfanikiwe
Tazama kadi
Malipo huwa ni kutokana na matendo. Chochote unacho tenda utavuna. Zingatia hatima ya kila aliye ipuuza haki ilikuwaje na jifunze kwa walio kutangulia. MAZINGATIO: Akhera ni uadilifu tu!
Sala si kwamba ni ibada tu bali ni ngao inayo tulinda na kuingia katika maasi. Basi, kuwa mwingi wa kumkumbuka na kumtaja sana Allah ili upate nguvu ya kiimani na utashi wa kweli. MAZINGATIO: Sala ndiyo uhai wa dhikri
Utafika muda wa kila mtu kuona uhalisia wa mambo kwa uwazi, lakini hapatokuwa na muda wa kutenda mema tena! Yakini ya kweli ni kuamini mwenyewe kwa hiyari kabla ya kufika muda wa kulazimika kuamini hali ya kuwa imani hiyo haitosaidia chochote. MAZINGATIO: Ni muhimu kuwa na yakini ya siku ya kiama.
Na wanapoambiwa msifanye uharibifu ardhini wanasema: Hapana, bali sisi niwafanyaji mazuriElewa! Kwa yakini, wao ndio waharibifu hasa na lakini hawatambui
Na yote haya tunakusimulia miongoni mwa habari za Mitume yale yanayoupa nguvu moyo wako. Na katika haya imekujia haki na mawaidha na ukumbusho kwa waumini
Kurukuu na kusujudu ni alama kubwa ya kuonesha unyenyekevu wetu kwa Allah. Fanya mema, kwani mafanikio yako yapo katika kumtii Allah na kufanya matendo mema. MAZINGATIO: Ibada ni utiifu.