Enyi mlio amini! Rukuuni na msujudu, na muabuduni Mola wenu Mlezi, na tendeni mema, ili mfanikiwe
Tazama kadi
Soma uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini kumtaja Allah ndilo jambo kubwa kabisa. Na Allah anayajua mnayo yatenda
Uhalisia wa mambo utakapo bainishwa baada ya muda wake kufika, haitobakia kwa mtu ila ni majuto tu. Kumbuka kuwa imani haitomfaa mtu baada ya muda wa kufanya matendo kuisha, fanya haraka kutenda mema kabla hujasema: “Najuta, laiti ninge……” MAZINGATIO: Kumbuka maisha ya baada ya kifo
Utafika muda wa kila mtu kuona uhalisia wa mambo kwa uwazi, lakini hapatokuwa na muda wa kutenda mema tena! Yakini ya kweli ni kuamini mwenyewe kwa hiyari kabla ya kufika muda wa kulazimika kuamini hali ya kuwa imani hiyo haitosaidia chochote. MAZINGATIO: Ni muhimu kuwa na yakini ya siku ya kiama.
Imani yako inakamilika kwa kufanya matendo mema na ibada kwa ikhlaswi. Kila jambo jema unalo jikurubisha nalo kwa ajili ya Allah ni ufunguo wa mafanikio. MAZINGATIO: Kutenda mema ni katika imani.
Kufuata matamanio ya nafsi inaweza kuwa sababu ya upotofu, basi usiisahau siku ya hesabu (siku ya kiyama). Ishi maisha yako yote kwa kuafikiana na yale anayo yaridhia Allah, ili ufanikiwe katika dunia na akhera. MAZINGATIO: Zingatia sana maisha ya akhera ili upate uongofu
Kufuata matamanio ya nafsi ni chanzo cha kukuweka mbali na njia sahihi, basi usiyaendekeze matamanio yako yakuongoze kwenye upotofu. Kumbuka kuwa Akhera kuna hesabu na adhabu, kuwa Mwangalifu! MAZINGATIO: Ni muhimu kuwa na tafakuri ya kina kuhusu hatma ya kufuata matamanio