Enyi mlio amini! Rukuuni na msujudu, na muabuduni Mola wenu Mlezi, na tendeni mema, ili mfanikiwe
Tazama kadi
Katika visa vya Mitumekuna mazingatio makubwa kwetu sisi wote. Ndani yake kuna ukumbusho wa kuzingatia na mafundisho kwa yaliyo tokea kwa wale walio tangulia. Qur’an siyo kitabu cha mazungumzo tu, bali ni kitabu cha ukweli, muongozo na rehma. MAZINGATIO: Ni muhimu kuwa na mazingatio katika visa vya wale walio tutangulia
Sala si kwamba ni ibada tu bali ni ngao inayo tulinda na kuingia katika maasi. Basi, kuwa mwingi wa kumkumbuka na kumtaja sana Allah ili upate nguvu ya kiimani na utashi wa kweli. MAZINGATIO: Sala ndiyo uhai wa dhikri
Kila nafsi itavuna ilicho chuma. Na mateso ya duniani ni matokeo ya dhulma za mwanaadam kujidhulumu mwenyewe. Allah hamdhulumu yeyote, lakini watu ndiyo wanaojidhulumu wenyewe. MAZINGATIO: Uadilifu wa Allah na hatari ya dhulma.
Soma uliyo funuliwa katika Kitabu, na ushike Sala. Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu. Na kwa yakini kumtaja Allah ndilo jambo kubwa kabisa. Na Allah anayajua mnayo yatenda
Kufuata matamanio ya nafsi inaweza kuwa sababu ya upotofu, basi usiisahau siku ya hesabu (siku ya kiyama). Ishi maisha yako yote kwa kuafikiana na yale anayo yaridhia Allah, ili ufanikiwe katika dunia na akhera. MAZINGATIO: Zingatia sana maisha ya akhera ili upate uongofu
Na yote haya tunakusimulia miongoni mwa habari za Mitume yale yanayoupa nguvu moyo wako. Na katika haya imekujia haki na mawaidha na ukumbusho kwa waumini