Enyi mlio amini! Rukuuni na msujudu, na muabuduni Mola wenu Mlezi, na tendeni mema, ili mfanikiwe
Tazama kadi
Ni nani atakaye tamani kurudi duniani bila ya kujua mafikio yake ya Akhera?! Maisha ya dunia ndiyo fursa nzuri ya kutenda, ambayo haina badala. Matendo yako ya sasa ndiyo yatakuwa kipimo cha mafikio yako katika siku ya ahadi (kiyama). MAZINGATIO: Akhera inahitajia kufikiria kabla ya kujuta.
Mpaka yanapo mfikia mmoja wao mauti, husema: Mola wangu Mlezi! NirudisheIli nitende mema sasa badala ya yale niliyo yaacha. Wapi! Hii ni kauli aisemayo yeye tu. Na nyuma yao kipo kizuizi mpaka siku watakapo fufuliwa
Kurukuu na kusujudu ni alama kubwa ya kuonesha unyenyekevu wetu kwa Allah. Fanya mema, kwani mafanikio yako yapo katika kumtii Allah na kufanya matendo mema. MAZINGATIO: Ibada ni utiifu.
Na wanapoambiwa msifanye uharibifu ardhini wanasema: Hapana, bali sisi niwafanyaji mazuriElewa! Kwa yakini, wao ndio waharibifu hasa na lakini hawatambui
Qur’an na Sala ni miongoni mwa ibada zenye athari kubwa katika maisha yetu. Ibada hizo mbili ni taa inayo angaza njia. Na sala ni ibada maalumu ambayo inatukataza tusifanye uchafu na maovu. Na ibada ya dhikri (kumkumbuka na kumtaja Allah) inaufanya moyo kuwa na utukufu na kuufungamanisha na Allah daima. MAZINGATIO: Dhikri na Sala ni miongoni m...
Usidai kuwa unatengeneza hali ya kuwa unapandikiza uharibifu (ufisadi). Mwanadamu anatakiwa kufikiria na kupima matendo yake kabla ya kujiridhisha kuwa anayo yafanya ni kheri. MAZINGATIO: Kuwa na fikra nzuri katika kutenda mema