Enyi mlio amini! Rukuuni na msujudu, na muabuduni Mola wenu Mlezi, na tendeni mema, ili mfanikiwe
Tazama kadi
Malipo huwa ni kutokana na matendo. Chochote unacho tenda utavuna. Zingatia hatima ya kila aliye ipuuza haki ilikuwaje na jifunze kwa walio kutangulia. MAZINGATIO: Akhera ni uadilifu tu!
Ni nani atakaye tamani kurudi duniani bila ya kujua mafikio yake ya Akhera?! Maisha ya dunia ndiyo fursa nzuri ya kutenda, ambayo haina badala. Matendo yako ya sasa ndiyo yatakuwa kipimo cha mafikio yako katika siku ya ahadi (kiyama). MAZINGATIO: Akhera inahitajia kufikiria kabla ya kujuta.
Kuna siku itakayo tokea ndani yake mambo ambayo mtu hajawahikufikiria kuwa yatatokea, kipindi cha watu watakapo fufuliwa kutoka makaburini mwao na kuanza kuuliza: “Nani aliye tufufua? Kukumbuka nguvu za Allah na uwezo wake katika siku ambayo majuto hayatomfaa mtu, hili ni jambo muhimu sana. MAZINGATIO: Ni muhimu kuamini siku ya kiama na ku...
Na yote haya tunakusimulia miongoni mwa habari za Mitume yale yanayoupa nguvu moyo wako. Na katika haya imekujia haki na mawaidha na ukumbusho kwa waumini
Utafika muda wa kila mtu kuona uhalisia wa mambo kwa uwazi, lakini hapatokuwa na muda wa kutenda mema tena! Yakini ya kweli ni kuamini mwenyewe kwa hiyari kabla ya kufika muda wa kulazimika kuamini hali ya kuwa imani hiyo haitosaidia chochote. MAZINGATIO: Ni muhimu kuwa na yakini ya siku ya kiama.
Katika kipindi ambacho mtu anafikiwa na kifo, hutamani kurudishwa duniani ili afanye matendo mema, lakini wapi, hakuna tena muda wa kupewa kwa ajili ya tamaa hiyo. Muda ni wa thamani,usisubiri kutenda mema mpaka kiama kikukute. MAZINGATIO: Toba ina muda wake, tumia fursa hiyo haraka kabla ya kuisha