Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi
Tazama kadi
Ujumbe wa Qur’an haubadilishi tu anuani, bali unamuokoa mwanaadam kutokana na ujinga. MAZINGATIO: Ujumbe wa Qur’an ni suluhisho la matatizo yote.
Qur’an si maneno yanayo somwa tu, bali ni mawaidha yanayozindua, na ponyo inayo maliza matatizo, na rahma inayo ulinda moyo wako kwa njia ya upole. MAZINGATIO: Nuru ya Qur’an ni yenye kuangaza katika kila tatizo
Qur’an siyo majibu yaliyo andaliwa tu, bali ni nuru inayo ambatana nawe hali ya kuwa nawe unaitafuta. MAZINGATIO: Qur’an ni nuru ya uongofu
Unapompenda Allah kwa dhati ya ukweli, hauhitajiki kufanya kazi ya ushawishi ili ukubaliwe na watu, bali Allah mwenyewe mwingi wa rehema atakupa upendo wake kwa hali usiyo itegemea na kukupa mafanikio makubwa katika maisha. MAZINGATIO: Mapenzi ya Allah, Mwingi wa rehema ni makubwa kuliko chochote
Unapo mchagua Allah kiukweli ina maanisha unakuwa umejipa uhuru wa kutokuwa mtumwa kwa yoyote. MAZINGATIO: Ni wajibu kuwa na tawhidi
Na siku tutakayomfufua shahidi (Mtume) katika kila umma kutoka miongoni mwao atakayethibitisha (kuwa aliwafikishia ujumbe wa Allah wakampinga), na tutakuleta wewe kuwa shahidi wa (watu) hawa. Na tumekuteremshia kitabu kikibainisha kila kitu, na rehema na bishara kwa Waislamu