Na wale (wenye akili ndio) ambao huyaunga aliyoamrisha Allah yaungwe, na wanaihofu hesabu mbaya
Tazama kadi
Na (kumbukeni) Tulipochukua ahadi kwa Wana wa Israeli kwamba, hamtamuabudu yeyote Ila Allah tu, na mtawatendea wema wazazi, na ndugu na yatima na maskini, na mseme na watu kwa maneno mazuri. Na simamisheni Swala na toeni Zaka, kisha mkakengeuka isipokuwa wachache tu kati yenu, na ilhali nyinyi mnapuuza
Watakapokujia wanafiki wanasema: Tunashuhudia kwamba wewe bila ya shaka yoyote ni Mtume wa Allah. Na Allah Anajua kuwa hakika wewe ni Mtume Wake, na Allah anashuhudia kuwa kwa hakika kabisa wanafiki ni waongo
Waambie waja wangu waseme maneno mazuri, maana Shetani huchochea ugomvi baina yao. Hakika Shetani ni adui aliye dhaahiri kwa mwanaadamu
Vipi (makafiri) waheshimu ahadi na makubaliano) na ilhali wakikushindeni hawatazami (hawajali) kwenu udugu wala ahadi[1]. Wanawafurahisheni kwa vinywa vyao tu (kwa maneno matamu), na ilhali nyoyo zao zinakataa. Na wengi wao ni waovu
Wanafiki hufanya matendo dhidi ya haki, wana amrishana maovu, na kupambana dhidi ya mema, na kumsahau Allah hatimaye Allah naye anawatelekeza katika uovu wao. Hivyo, ni wajibu kuwa na tahadhari ya unafiki katika maneno na matendo, na tuhakikishe tunadumu katika kutakasa matendo yetu kwa ajili ya Allah. Tunachojifunza: Hatari ya unafiki,...
Wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa Motoni, kwa sababu ya mioyo yao kuficha ukafiri na kudhihirisha imani kwa uongo. Basi, Waislamu wawe na tahadhari kubwa ya kujionesha na kufanya unafiki katika maneno na matendo. Na ni wajibu kuwa na nia ya kweli na kushikamana na imani kwani ndiyo msingi mkuu wa maisha yetu. Tunachojifunza: Tahad...