Na wale (wenye akili ndio) ambao huyaunga aliyoamrisha Allah yaungwe, na wanaihofu hesabu mbaya
Tazama kadi
Sema: Kwa hakika Mola wangu Mlezi humkunjulia riziki na humdhikisha amtakaye katika waja wake. Na chochote mtakacho kitoa Yeye atakilipa. Naye ni Mbora wa wanao ruzuku
Allah Mtukufu ametuumba mataifa na makabila mbali mbali ili tujuane sisi kwa sisi. Kutofautiana kimaumbile na kimaeneo ni neema, na si sababu ya kutengana. Bali iwe ni msingi wa kuboresha mahusiano yetu kwa kuheshimiana na kutambuana. Tunachojifunza: Kuishi pamoja kwa amani, na kuthaminiana kibinaadamu ni katika Uislamu.
Je, Huwaoni wanao fanya unaafiki na wanawaambia ndugu zao walio kufuru katika Watu wa Kitabu: Mkitolewa na sisi lazima tutatoka pamoja nanyi, wala hatutamt’ii yeyote kabisa dhidi yenu. Na mkipigwa vita lazima tutakusaidieni. Na Mwenyezi Mungu anashuhudia kuwa hakika hao bila ya shaka ni waongo
Na mwabuduni Allah na msikishirikishe naye kitu chochote. Na wazazi wawili wafanyieni mazuri, na ndugu wa karibu (wa nasaba), na Yatima na maskini na jirani wa karibu (mwenye udugu wa nasaba) na jirani wa mbali (kwa makazi au udugu) na rafiki aliyeko ubavuni (rafiki mwenye usuhuba wa karibu na pia mke) na msafiri (aliyeharibikiwa) na wale walio chi...
Kumfanyia wema jirani ni miongoni mwa tabia njema zilizo sisitizwa na dini yetu tukufu ya Uislamu.Haki za jirani, haziishii kwa jirani aliye ndugu tu, bali zimekusanya hata jirani wa mbali. Hivyo basi, ni wajibu wetu kuzifanya rehema za Allah na uadilifu wake ndiyo msingi wa kuamiliana kwetu katika maisha yetu ya kila siku.Tunachojifunza...
Enyi watu, mcheni Mola wenu Mlezi Ambaye amekuumbeni kutokana na nafsi moja tu na ameumba kutoka kwenye nafsi hiyo mke wake (Hawaa), na akaeneza kutokana na wawili hao wanaume wengi na wanawake (wengi), na mcheni Allah Ambaye mnaombana kupitia yeye, na (ogopeni kukata) udugu. Hakika, Allah amekuwa Mwenye kukufuatilieni kwa karibu sana