Na wale (wenye akili ndio) ambao huyaunga aliyoamrisha Allah yaungwe, na wanaihofu hesabu mbaya
Tazama kadi
Kumfanyia wema jirani ni miongoni mwa tabia njema zilizo sisitizwa na dini yetu tukufu ya Uislamu.Haki za jirani, haziishii kwa jirani aliye ndugu tu, bali zimekusanya hata jirani wa mbali. Hivyo basi, ni wajibu wetu kuzifanya rehema za Allah na uadilifu wake ndiyo msingi wa kuamiliana kwetu katika maisha yetu ya kila siku.Tunachojifunza...
Kufurahi kwetu kwa neema alizo tuneemesha Allah juu yetu ni miongoni mwa fadhila zake na rehema zake, na hivyo ni bora kuliko chochote tunacho kikusanya katika dunia. Ni wajibu wetu kuwa wenye shukurani, na kukumbuka siku zote kuwa radhi za Allah ni neema kubwa. Tunachojifunza: Fadhila za Allah, kuridhia na kuwa na shukurani juu ya neema...
Na mwabuduni Allah na msikishirikishe naye kitu chochote. Na wazazi wawili wafanyieni mazuri, na ndugu wa karibu (wa nasaba), na Yatima na maskini na jirani wa karibu (mwenye udugu wa nasaba) na jirani wa mbali (kwa makazi au udugu) na rafiki aliyeko ubavuni (rafiki mwenye usuhuba wa karibu na pia mke) na msafiri (aliyeharibikiwa) na wale walio chi...
Ukweli ni njia ya wokovu Tunatakiwa kushikamana na wakweli, kwani ndiyo salama ya nyoyo zetu na ukweli wa maneno: “ Mcheni Allah, na kuweni pamoja na wakweli” ili muishi maisha yaliyo jaa baraka na uongofu. Tunachojifunza: Umuhimu wa Ukweli, toba na imani
Na wanapokutana na walioamini wanasema: Tumeamini. Na wanapokuwa faragha na mashetani wao wanasema: Sisi tuko pamoja nanyi, tunachokifanya sisi tunacheza shere tu
Sema: Kwa hakika Mola wangu Mlezi humkunjulia riziki na humdhikisha amtakaye katika waja wake. Na chochote mtakacho kitoa Yeye atakilipa. Naye ni Mbora wa wanao ruzuku