Je! Umemwona aliye yafanya matamanio yake kuwa ndio mungu wake? Basi je, wewe utakuwa ni wakili wake?
Tazama kadi
Matamanio huvutia nyoyo kupenda mali, watoto na vipambo vya dunia(wanawake nk) lakini vyote hivyo ni starehe ya muda tu. Ama marejeo mema yapo kwa Allah kwa kila mwenye kutakasa niya na kufanya juhudi. Tunajifunza kuwa: Kutakasa niya, ndiyo mafanikio ya kweli.
Wakati mawimbi yanapo zidi, na hali ya hewa ikawa mbaya baharini, huwa tunauona udhaifu wetu mbele ya uwezo wa Allah, na huwa tunamuelekea Yeye kwa kumuomba kwa ikhlaswi. Lakini balaa kubwa ni pale tunapo okolewa na kuwa salama, kuacha kuonesha shukurani zetu kwa Allah, jambo hili ni baya sana na lisilo faa kufanywa na Waumini wa kweli. Tunajifunz...
Na wanapo sikia upuuzi hujitenga nao na husema: Sisi tuna vitendo vyetu, na nyinyi mna vitendo vyenu. Salamun Alaikum, Amani juu yenu! Sisi hatutaki kujibizana na wajinga
Kujiepusha na upuuzi ni miongoni mwa tabia njema za waja wa Allah. Hivyo, tunawajibika kuwajibu wajinga, wanapo tusemeza ubaya: “Sisi tuna vitendo vyetu na nyinyi mna vitendo vyenu, hatutaki mijadala na wajinga”. Tunajifunza kuwa: Amani ndio njia yetu, na adabu bora ya kujitenga na upuuzi ni amani.
Pepo si ya mwenye kuzuia hasira zake tu, bali ni ya mwenye kutoa katika wasaa na dhiki, na akawasamehe watu. Njia za kupata radhi za Allah zipo katika matendo ya wema.Tunajifunza kuwa: Huruma ni katika matendo ya wema.
Mema na maovu hayalingani. Kuwa miongoni mwa wale ambao wanalipiza ubaya kwa wema. Huwenda adui yako akabadilika na kuwa rafiki yako kipenzi. Na haya hawayafikii ila walio na subira na wenye bahati kubwa. Tunajifunza kuwa: Wema na subira ni katika tabia njema za Uislamu