Huu ni ubainifu kwa watu, na ni uongofu na ni mawaidha kwa wacha Mungu
Tazama kadi
Unaweza kuwa hauhitaji mawaidha marefu, bali Aya moja tu, ikaingia kwenye moyo wako ulio kuwa tayari, na ikabadilisha mwenendo wako wa maisha! MAZINGATIO: Moyo wenye Imani huzinduka kwa Qur’an
Na Hakika Tumeirahisisha Qur’an Kwa Ajili Ya Ukumbusho Je Kuna Mwenye kukumbuka? Kina ‘Aad walikadhibisha, basi vipi ilikuwa adhabu Yangu na maonyo Yangu? Hakika Sisi Tumewapelekea upepo wa kimbunga wenye sauti kali na baridi kali katika siku korofi yenye kuendelea mfululizo Unawang’oa watu kana kwamba vigogo vya mtende vilong’olewa Basi vipi i...
Kuihama Qur’an haimaanishi kuisahau tu, bali kuishi kwa kujiona kuwa Qur’an haituhusu kwa lolote! MAZINGATIO: Usiihame Qur’an!
Wakati mwingine hauhitaji jibu…. Bali Mwangaza tu! Basi, tambua kuwa umeshakujia mwangaza kutoka kwa Allah unao ujaza moyo wako utulivu na matumaini makubwa. MAZINGATIO: Ni wajibu kuzingatia mwangaza wa Qur’an
Unaweza kuwa gizani kwa muda mrefu.. Lakini mwangaza haupo mbali. Allah ndiye Msimamizi wa waja wake, na Yeye ndiye huwatoa gizani na kuwaingiza kwenye mwangaza. MAZINGATIO: Safari ya kupata mwangaza ni hatua.
Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, chenye baraka, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili