Huu ni ubainifu kwa watu, na ni uongofu na ni mawaidha kwa wacha Mungu
Tazama kadi
Enyi Watu wa Kitabu, kwa hakika kabisa, amekujieni Mtume wetu (Muhammad) akikuwekeeni wazi mengi mliyokuwa mkiyaficha katika Kitabu (Taurati na Injili) na akisamehe mengi. Bila shaka, imekujiieni nuru kutoka kwa Allah na Kitabu kinachobainisha Kwa (Kitabu) hicho Allah anamuongoza anayefuata radhi zake katika njia za amani na anawatoa katika viza (...
Allah ni Mwenye kuwanusuru wale walioamini; huwatoa gizani na kuwapeleka kwenye mwangaza. Na ambao wamekufuru, watetezi wao ni Matwaghuti; huwatoa katika nuru na kuwaingiza kwenye giza. Hao ndio watu wa Motoni, wao humo watasalia milele
Wakati mwingine hauhitaji jibu…. Bali Mwangaza tu! Basi, tambua kuwa umeshakujia mwangaza kutoka kwa Allah unao ujaza moyo wako utulivu na matumaini makubwa. MAZINGATIO: Ni wajibu kuzingatia mwangaza wa Qur’an
Siyo lazima ujue kila kitu. Inakutosha tu kuufungua moyo wako. Allah amekiwepesisha Kitabu chake Kitukufu(Qur’an) kwa kila mwenye kutaka mafanikio. MAZINGATIO: Qur’an ni mwangaza kwa mwenye kuutafuta.
Njia zote zinaweza kukupoteza, isipo kuwa njia moja tu, iliyo dhaminiwa na Allah mwenyewe, alipo sema: “Basi atakaye ufuata uwongofu wangu, hatapotea wala hatataabika”. MAZINGATIO: Ni wajibu kufuata mwongozo wa Allah ili kupata mafanikio
Usipite kwenye Aya yoyote, bila ya mazingatio. Huenda haikuteremshwa kwa mwingine zaidi yako wewe tu, bali na kwa ajili yako tu! MAZINGATIO: Kuwa mwangalifu! Aya moja tu inaweza kukuzindua jambo muhimu katika Maisha yako