Huu ni ubainifu kwa watu, na ni uongofu na ni mawaidha kwa wacha Mungu
Tazama kadi
Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, chenye baraka, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili
Usiseme: “Qur’an ni ngumu”. Kwani Allah amekwisha kuwepesishia. Si kwa ajili ya kusomwa tu, bali hata kuuongoza moyo wako kwenye mafanikio ya kweli. Anza sasa! Utaona maajabu ya safari ya mafanikio yako. MAZINGATIO: Mafanikio yanapatikana kwa kufuata njia na muongozo wa Qur’an.
Enyi watu, hakika yamekujieni mawaidha kutoka kwa Mola wenu Mlezi na ponyo (dawa) ya (maradhi) yaliyomo vifuani (mwenu) na muongozo na rehema kwa Waumini
Qur’an haikuteremshwa ili kuwa mapambio ya vitu, bali imeteremshwa ili kuziongoza nyoyo. Fungua moyo wako kwanza kabla ya kuufungua msahafu wakati wa kuusoma! MAZINGATIO: Ni wajibu kuizingatia Qur’an.
Unaweza kuwa gizani kwa muda mrefu.. Lakini mwangaza haupo mbali. Allah ndiye Msimamizi wa waja wake, na Yeye ndiye huwatoa gizani na kuwaingiza kwenye mwangaza. MAZINGATIO: Safari ya kupata mwangaza ni hatua.
Na Hakika Tumeirahisisha Qur’an Kwa Ajili Ya Ukumbusho Je Kuna Mwenye kukumbuka? Kina ‘Aad walikadhibisha, basi vipi ilikuwa adhabu Yangu na maonyo Yangu? Hakika Sisi Tumewapelekea upepo wa kimbunga wenye sauti kali na baridi kali katika siku korofi yenye kuendelea mfululizo Unawang’oa watu kana kwamba vigogo vya mtende vilong’olewa Basi vipi i...