Huu ni ubainifu kwa watu, na ni uongofu na ni mawaidha kwa wacha Mungu
Tazama kadi
Kuihama Qur’an haimaanishi kuisahau tu, bali kuishi kwa kujiona kuwa Qur’an haituhusu kwa lolote! MAZINGATIO: Usiihame Qur’an!
Kwa hakika kabisa, Waumini (kamili) ni wale ambao anapotajwa Allah nyoyo zao hujaa hofu, na wanaposomewa Aya zake huwaongezea imani, na wanamtegemea Mola wao Mlezi tu
Qur’an haifiki kwako kama fikra ya ghafla, bali inafika kama mvua inayo huisha yale yote uliyo kuwa unadhania kuwa yame toweka kwako. MAZINGATIO: Ni wajibu kuuitikia wito wa Qur’an unapo kufikia
Kama vile Aya zote zimekuwa zikikusubiria wewe kwa Subira! Mpaka ukafika wakati wake kwako, zika angaza moyoni mwako, bila ya kuonwa na yeyote zaidi yako, basi zinduka! MAZINGATIO: Allah ana makusudio yake mazuri kwako, kupitia Aya zake
Usipite kwenye Aya yoyote, bila ya mazingatio. Huenda haikuteremshwa kwa mwingine zaidi yako wewe tu, bali na kwa ajili yako tu! MAZINGATIO: Kuwa mwangalifu! Aya moja tu inaweza kukuzindua jambo muhimu katika Maisha yako
Qur’an haigongi masikio yako, bali inaugonga moyo wako, ikiwa uta ufungua, basi utasikia mazuri ambayo haujawahi kuyasikia kabla yake! MAZINGATIO: Kuwa mwepesi wa kuisikiliza Qur’an ii unufaike kwayo