Enyi mlio amini! Rukuuni na msujudu, na muabuduni Mola wenu Mlezi, na tendeni mema, ili mfanikiwe
Tazama kadi
Qur’an na Sala ni miongoni mwa ibada zenye athari kubwa katika maisha yetu. Ibada hizo mbili ni taa inayo angaza njia. Na sala ni ibada maalumu ambayo inatukataza tusifanye uchafu na maovu. Na ibada ya dhikri (kumkumbuka na kumtaja Allah) inaufanya moyo kuwa na utukufu na kuufungamanisha na Allah daima. MAZINGATIO: Dhikri na Sala ni miongoni m...
Katika kipindi ambacho mtu anafikiwa na kifo, hutamani kurudishwa duniani ili afanye matendo mema, lakini wapi, hakuna tena muda wa kupewa kwa ajili ya tamaa hiyo. Muda ni wa thamani,usisubiri kutenda mema mpaka kiama kikukute. MAZINGATIO: Toba ina muda wake, tumia fursa hiyo haraka kabla ya kuisha
Kila nafsi itavuna ilicho chuma. Na mateso ya duniani ni matokeo ya dhulma za mwanaadam kujidhulumu mwenyewe. Allah hamdhulumu yeyote, lakini watu ndiyo wanaojidhulumu wenyewe. MAZINGATIO: Uadilifu wa Allah na hatari ya dhulma.
Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya wewe uwe Khalifa (kiongozi) katika ardhi. Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio yakakupoteza kwenye Njia ya Allah. Hakika wanao ipotea Njia ya Allah wakaiacha, watapata adhabu kali kwasababu ya kusahau kwao Siku ya Hesabu
Basi kila mmoja tulimtesa kwa mujibu wa makosa yake. Kati yao wapotulio wapelekea kimbunga cha changarawe; na kati yao wapo walio nyakuliwa na ukelele; na kati yao wapo ambao tulio wadidimiza katika ardhi; na kati yao wapo tulio wazamisha. Wala Allah hakuwa mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa wenyewe wakijidhulumu nafsi zao
Katika kila habari miongoni mwa habari za mitume tunapata mambo yanayo thibitisha imani zetu na uongofu wa nyoyo. Qur’an ni ukumbusho na nuru kwa waumini wa kila zama. MAZINGATIO: Haki ya wazi inapatikana ndani ya masomo ya Qur’an.