Enyi mlio amini! Rukuuni na msujudu, na muabuduni Mola wenu Mlezi, na tendeni mema, ili mfanikiwe
Tazama kadi
Kila kisa katika Qur’an kimebeba masomo kwetu ya kweli katika maisha. Kwa kila mwenye kumuamini Allah atapata kwenye kila Aya muongozo na rehma. MAZINGATIO: Qur’an ni muongozo na masomo ya kimaisha.
Katika kipindi ambacho mtu anafikiwa na kifo, hutamani kurudishwa duniani ili afanye matendo mema, lakini wapi, hakuna tena muda wa kupewa kwa ajili ya tamaa hiyo. Muda ni wa thamani,usisubiri kutenda mema mpaka kiama kikukute. MAZINGATIO: Toba ina muda wake, tumia fursa hiyo haraka kabla ya kuisha
Mpaka yanapo mfikia mmoja wao mauti, husema: Mola wangu Mlezi! NirudisheIli nitende mema sasa badala ya yale niliyo yaacha. Wapi! Hii ni kauli aisemayo yeye tu. Na nyuma yao kipo kizuizi mpaka siku watakapo fufuliwa
Kurukuu na kusujudu ni alama kubwa ya kuonesha unyenyekevu wetu kwa Allah. Fanya mema, kwani mafanikio yako yapo katika kumtii Allah na kufanya matendo mema. MAZINGATIO: Ibada ni utiifu.
Na wanapoambiwa msifanye uharibifu ardhini wanasema: Hapana, bali sisi niwafanyaji mazuriElewa! Kwa yakini, wao ndio waharibifu hasa na lakini hawatambui
Na ungeliwaona wakosefu wanvyo inamisha vichwa vyao mbele ya Mola wao Mlezi, (wakisema): Mola wetu Mlezi! Tumeshaona, na tumeshasikia. Turejeshe tukatende mema, kwani hakika sisi tumekwisha kuwa na yakini sasa