Enyi mlio amini! Rukuuni na msujudu, na muabuduni Mola wenu Mlezi, na tendeni mema, ili mfanikiwe
Tazama kadi
Utafika muda wa kila mtu kuona uhalisia wa mambo kwa uwazi, lakini hapatokuwa na muda wa kutenda mema tena! Yakini ya kweli ni kuamini mwenyewe kwa hiyari kabla ya kufika muda wa kulazimika kuamini hali ya kuwa imani hiyo haitosaidia chochote. MAZINGATIO: Ni muhimu kuwa na yakini ya siku ya kiama.
Imani yako inakamilika kwa kufanya matendo mema na ibada kwa ikhlaswi. Kila jambo jema unalo jikurubisha nalo kwa ajili ya Allah ni ufunguo wa mafanikio. MAZINGATIO: Kutenda mema ni katika imani.
Basi kila mmoja tulimtesa kwa mujibu wa makosa yake. Kati yao wapotulio wapelekea kimbunga cha changarawe; na kati yao wapo walio nyakuliwa na ukelele; na kati yao wapo ambao tulio wadidimiza katika ardhi; na kati yao wapo tulio wazamisha. Wala Allah hakuwa mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa wenyewe wakijidhulumu nafsi zao
Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya wewe uwe Khalifa (kiongozi) katika ardhi. Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio yakakupoteza kwenye Njia ya Allah. Hakika wanao ipotea Njia ya Allah wakaiacha, watapata adhabu kali kwasababu ya kusahau kwao Siku ya Hesabu
Kufuata matamanio ya nafsi inaweza kuwa sababu ya upotofu, basi usiisahau siku ya hesabu (siku ya kiyama). Ishi maisha yako yote kwa kuafikiana na yale anayo yaridhia Allah, ili ufanikiwe katika dunia na akhera. MAZINGATIO: Zingatia sana maisha ya akhera ili upate uongofu
Na ungeliwaona wakosefu wanvyo inamisha vichwa vyao mbele ya Mola wao Mlezi, (wakisema): Mola wetu Mlezi! Tumeshaona, na tumeshasikia. Turejeshe tukatende mema, kwani hakika sisi tumekwisha kuwa na yakini sasa