Enyi mlio amini! Rukuuni na msujudu, na muabuduni Mola wenu Mlezi, na tendeni mema, ili mfanikiwe
Tazama kadi
Katika kipindi ambacho baadhi ya watu wanadai kuwa wanafanya wema, hali ya kuwa kiuhalisia wao ndiyo wanao fanya uharibifu. Haya huyajua ukweli wake kwa uwazi wale wenye kuzingatia mambo. MAZINGATIO: Umuhimu wa kujua ukweli na ufisadi
Utafika muda wa kila mtu kuona uhalisia wa mambo kwa uwazi, lakini hapatokuwa na muda wa kutenda mema tena! Yakini ya kweli ni kuamini mwenyewe kwa hiyari kabla ya kufika muda wa kulazimika kuamini hali ya kuwa imani hiyo haitosaidia chochote. MAZINGATIO: Ni muhimu kuwa na yakini ya siku ya kiama.
Kwa hakika kabisa, katika simulizi zao (hao Mitume) kuna mazingatio kwa wenye akili. Haikuwa (hii Qur’an ni) maneno yanayozushwa lakini ni usadikisho (uthibitisho) wa (maandiko matakatifu) yaliyokuwepo kabla yake (Taurati na Injili) na ni ufafanuzi wa kila kitu na ni muongozo na rehema kwa watu wanaoamini
Ni nani atakaye tamani kurudi duniani bila ya kujua mafikio yake ya Akhera?! Maisha ya dunia ndiyo fursa nzuri ya kutenda, ambayo haina badala. Matendo yako ya sasa ndiyo yatakuwa kipimo cha mafikio yako katika siku ya ahadi (kiyama). MAZINGATIO: Akhera inahitajia kufikiria kabla ya kujuta.
Kuna siku itakayo tokea ndani yake mambo ambayo mtu hajawahikufikiria kuwa yatatokea, kipindi cha watu watakapo fufuliwa kutoka makaburini mwao na kuanza kuuliza: “Nani aliye tufufua? Kukumbuka nguvu za Allah na uwezo wake katika siku ambayo majuto hayatomfaa mtu, hili ni jambo muhimu sana. MAZINGATIO: Ni muhimu kuamini siku ya kiama na ku...
Basi kila mmoja tulimtesa kwa mujibu wa makosa yake. Kati yao wapotulio wapelekea kimbunga cha changarawe; na kati yao wapo walio nyakuliwa na ukelele; na kati yao wapo ambao tulio wadidimiza katika ardhi; na kati yao wapo tulio wazamisha. Wala Allah hakuwa mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa wenyewe wakijidhulumu nafsi zao