Enyi mlio amini! Rukuuni na msujudu, na muabuduni Mola wenu Mlezi, na tendeni mema, ili mfanikiwe
Tazama kadi
Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya wewe uwe Khalifa (kiongozi) katika ardhi. Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio yakakupoteza kwenye Njia ya Allah. Hakika wanao ipotea Njia ya Allah wakaiacha, watapata adhabu kali kwasababu ya kusahau kwao Siku ya Hesabu
Katika visa vya Mitumekuna mazingatio makubwa kwetu sisi wote. Ndani yake kuna ukumbusho wa kuzingatia na mafundisho kwa yaliyo tokea kwa wale walio tangulia. Qur’an siyo kitabu cha mazungumzo tu, bali ni kitabu cha ukweli, muongozo na rehma. MAZINGATIO: Ni muhimu kuwa na mazingatio katika visa vya wale walio tutangulia
Qur’an na Sala ni miongoni mwa ibada zenye athari kubwa katika maisha yetu. Ibada hizo mbili ni taa inayo angaza njia. Na sala ni ibada maalumu ambayo inatukataza tusifanye uchafu na maovu. Na ibada ya dhikri (kumkumbuka na kumtaja Allah) inaufanya moyo kuwa na utukufu na kuufungamanisha na Allah daima. MAZINGATIO: Dhikri na Sala ni miongoni m...
Basi kila mmoja tulimtesa kwa mujibu wa makosa yake. Kati yao wapotulio wapelekea kimbunga cha changarawe; na kati yao wapo walio nyakuliwa na ukelele; na kati yao wapo ambao tulio wadidimiza katika ardhi; na kati yao wapo tulio wazamisha. Wala Allah hakuwa mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa wenyewe wakijidhulumu nafsi zao
Malipo huwa ni kutokana na matendo. Chochote unacho tenda utavuna. Zingatia hatima ya kila aliye ipuuza haki ilikuwaje na jifunze kwa walio kutangulia. MAZINGATIO: Akhera ni uadilifu tu!
Katika kipindi ambacho baadhi ya watu wanadai kuwa wanafanya wema, hali ya kuwa kiuhalisia wao ndiyo wanao fanya uharibifu. Haya huyajua ukweli wake kwa uwazi wale wenye kuzingatia mambo. MAZINGATIO: Umuhimu wa kujua ukweli na ufisadi