Huu ni ubainifu kwa watu, na ni uongofu na ni mawaidha kwa wacha Mungu
Tazama kadi
Qur’an haifiki kwako kama fikra ya ghafla, bali inafika kama mvua inayo huisha yale yote uliyo kuwa unadhania kuwa yame toweka kwako. MAZINGATIO: Ni wajibu kuuitikia wito wa Qur’an unapo kufikia
Njia zote zinaweza kukupoteza, isipo kuwa njia moja tu, iliyo dhaminiwa na Allah mwenyewe, alipo sema: “Basi atakaye ufuata uwongofu wangu, hatapotea wala hatataabika”. MAZINGATIO: Ni wajibu kufuata mwongozo wa Allah ili kupata mafanikio
Kila Aya iliyo teremshwa imeletwa ili iufikie moyo wako. Na kila mawaidha yaliyomo ndani yake pia, ni kama vile yameandikwa kwa ajili yako peke yako, basi kuwa mwangalifu wa kuzingatia yaliyomo ndani yake. MAZINGATIO: Qur’an ni ujumbe maalumu kwako!
Aya siyo herufi za kuhifadhiwa tu, bali ni ujumbe kutoka mbinguni, zinazo takiwa kufahamika na kukubadilisha mienendo yako. MAZINGATIO: Ni wajibu kuishi kwa mujibu wa maelekezo ya Aya za Qur’an.
Unapo hisi siku yoyote kuwa upo peke yako gizani, basi kumbuka kuwa Allah ndiye Mlinzi, hadhaliliki yeyote mwenye kumtegemea Yeye. MAZINGATIO: Allah yu pamoja nawe kwa hali yoyote, basi Mtegemee Yeye tu!
Usipite kwenye Aya yoyote, bila ya mazingatio. Huenda haikuteremshwa kwa mwingine zaidi yako wewe tu, bali na kwa ajili yako tu! MAZINGATIO: Kuwa mwangalifu! Aya moja tu inaweza kukuzindua jambo muhimu katika Maisha yako