Huu ni ubainifu kwa watu, na ni uongofu na ni mawaidha kwa wacha Mungu
Tazama kadi
Unapo pata kujihisi moyo wako upo katika Aya aidi inapo somwa, basi tambua kuwa wewe upo karibu sana na msaada wa Allah zaidi ya unavyo dhania. MAZINGATIO: Utulize moyo wako katika Qur’an
Siyo lazima ujue kila kitu. Inakutosha tu kuufungua moyo wako. Allah amekiwepesisha Kitabu chake Kitukufu(Qur’an) kwa kila mwenye kutaka mafanikio. MAZINGATIO: Qur’an ni mwangaza kwa mwenye kuutafuta.
Fikiria, itakapo tokea jina lako kushitakiwa na Mtume wako, kwa sababu tu ya kukihama Kitabu cha Allah (Qur’an)!!! MAZINGATIO: Huu ni wito wa kurudi katika Qur’an.
Uovu si kukosa njia, bali ni kwa kuendelea kufuata njia iliyo mbali na mwangaza wa Allah! Basi, fuata uongofu, utapata utulivu daima. MAZINGATIO: Utulivu wa moyo upo katika kufuata uongofu wa Allah.
Kuihama Qur’an haimaanishi kuisahau tu, bali kuishi kwa kujiona kuwa Qur’an haituhusu kwa lolote! MAZINGATIO: Usiihame Qur’an!
Kama vile Aya zote zimekuwa zikikusubiria wewe kwa Subira! Mpaka ukafika wakati wake kwako, zika angaza moyoni mwako, bila ya kuonwa na yeyote zaidi yako, basi zinduka! MAZINGATIO: Allah ana makusudio yake mazuri kwako, kupitia Aya zake