Huu ni ubainifu kwa watu, na ni uongofu na ni mawaidha kwa wacha Mungu
Tazama kadi
Usiseme: “Qur’an ni ngumu”. Kwani Allah amekwisha kuwepesishia. Si kwa ajili ya kusomwa tu, bali hata kuuongoza moyo wako kwenye mafanikio ya kweli. Anza sasa! Utaona maajabu ya safari ya mafanikio yako. MAZINGATIO: Mafanikio yanapatikana kwa kufuata njia na muongozo wa Qur’an.
Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, chenye baraka, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili
Kama vile Aya zote zimekuwa zikikusubiria wewe kwa Subira! Mpaka ukafika wakati wake kwako, zika angaza moyoni mwako, bila ya kuonwa na yeyote zaidi yako, basi zinduka! MAZINGATIO: Allah ana makusudio yake mazuri kwako, kupitia Aya zake
Qur’an haikuteremshwa ili kuwa mapambio ya vitu, bali imeteremshwa ili kuziongoza nyoyo. Fungua moyo wako kwanza kabla ya kuufungua msahafu wakati wa kuusoma! MAZINGATIO: Ni wajibu kuizingatia Qur’an.
Na Hakika Tumeirahisisha Qur’an Kwa Ajili Ya Ukumbusho Je Kuna Mwenye kukumbuka? Kina ‘Aad walikadhibisha, basi vipi ilikuwa adhabu Yangu na maonyo Yangu? Hakika Sisi Tumewapelekea upepo wa kimbunga wenye sauti kali na baridi kali katika siku korofi yenye kuendelea mfululizo Unawang’oa watu kana kwamba vigogo vya mtende vilong’olewa Basi vipi i...
Usipite kwenye Aya yoyote, bila ya mazingatio. Huenda haikuteremshwa kwa mwingine zaidi yako wewe tu, bali na kwa ajili yako tu! MAZINGATIO: Kuwa mwangalifu! Aya moja tu inaweza kukuzindua jambo muhimu katika Maisha yako