Huu ni ubainifu kwa watu, na ni uongofu na ni mawaidha kwa wacha Mungu
Tazama kadi
Qur’an haikuteremshwa ili kuwa mapambio ya vitu, bali imeteremshwa ili kuziongoza nyoyo. Fungua moyo wako kwanza kabla ya kuufungua msahafu wakati wa kuusoma! MAZINGATIO: Ni wajibu kuizingatia Qur’an.
Kama vile Aya zote zimekuwa zikikusubiria wewe kwa Subira! Mpaka ukafika wakati wake kwako, zika angaza moyoni mwako, bila ya kuonwa na yeyote zaidi yako, basi zinduka! MAZINGATIO: Allah ana makusudio yake mazuri kwako, kupitia Aya zake
Siyo lazima ujue kila kitu. Inakutosha tu kuufungua moyo wako. Allah amekiwepesisha Kitabu chake Kitukufu(Qur’an) kwa kila mwenye kutaka mafanikio. MAZINGATIO: Qur’an ni mwangaza kwa mwenye kuutafuta.
Kuihama Qur’an haimaanishi kuisahau tu, bali kuishi kwa kujiona kuwa Qur’an haituhusu kwa lolote! MAZINGATIO: Usiihame Qur’an!
Uovu si kukosa njia, bali ni kwa kuendelea kufuata njia iliyo mbali na mwangaza wa Allah! Basi, fuata uongofu, utapata utulivu daima. MAZINGATIO: Utulivu wa moyo upo katika kufuata uongofu wa Allah.
Unaweza kuwa hauhitaji mawaidha marefu, bali Aya moja tu, ikaingia kwenye moyo wako ulio kuwa tayari, na ikabadilisha mwenendo wako wa maisha! MAZINGATIO: Moyo wenye Imani huzinduka kwa Qur’an