Huu ni ubainifu kwa watu, na ni uongofu na ni mawaidha kwa wacha Mungu
Tazama kadi
Usipite kwenye Aya yoyote, bila ya mazingatio. Huenda haikuteremshwa kwa mwingine zaidi yako wewe tu, bali na kwa ajili yako tu! MAZINGATIO: Kuwa mwangalifu! Aya moja tu inaweza kukuzindua jambo muhimu katika Maisha yako
Unapo hisi siku yoyote kuwa upo peke yako gizani, basi kumbuka kuwa Allah ndiye Mlinzi, hadhaliliki yeyote mwenye kumtegemea Yeye. MAZINGATIO: Allah yu pamoja nawe kwa hali yoyote, basi Mtegemee Yeye tu!
Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, chenye baraka, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili
Unaweza kuwa gizani kwa muda mrefu.. Lakini mwangaza haupo mbali. Allah ndiye Msimamizi wa waja wake, na Yeye ndiye huwatoa gizani na kuwaingiza kwenye mwangaza. MAZINGATIO: Safari ya kupata mwangaza ni hatua.
Allah ni Mwenye kuwanusuru wale walioamini; huwatoa gizani na kuwapeleka kwenye mwangaza. Na ambao wamekufuru, watetezi wao ni Matwaghuti; huwatoa katika nuru na kuwaingiza kwenye giza. Hao ndio watu wa Motoni, wao humo watasalia milele
Njia zote zinaweza kukupoteza, isipo kuwa njia moja tu, iliyo dhaminiwa na Allah mwenyewe, alipo sema: “Basi atakaye ufuata uwongofu wangu, hatapotea wala hatataabika”. MAZINGATIO: Ni wajibu kufuata mwongozo wa Allah ili kupata mafanikio